Featured

Loading...


Magufuli Akomalia Kauli Mbiu ya Magufuli For Change (M4C)


Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, ameendelea kujinadi katika kampeni zake, huku akitumia kauli mbiu ya Movement for Change (M4C) inayotumiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwenye mikutano yake.

Chadema hivi karibuni waliilalamikia hatua hiyo ya Dk. Magufuli na kumtaka aache kutumia kauli mbiu hiyo ambayo ina maana ya ‘vuguvugu la mabadiliko’, huku wakitishia kumpandisha kizimbani kwa kile walichoeleza ni alama yao waliyoisajili.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa mpira wa Kyerwa Mjini, mkoani Kagera juzi, mgombea huyo wa CCM aliuambia uliojitokeza kumsikiliza kuwa kama wanataka mabadiliko wamchague yeye kwasababu yeye ndiye mwenye uwezo wa kuleta mabadiliko ya kweli na kuibadilisha kauli mbiu hiyo kwa kuweka jina lake: Magufuli for Change (M4C).

“Mimi ni Magufuli for Change, haya imbeni Magufuli for Change,” aliwaambia wananchi hao ambao nao walianza kuimba wakimfuatisha.

Katika mkutano huo, Dk. Magufuli pia alimrushia kijembe Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, ambaye amekuwa akizunguka na mgombea urais aliyesimamishwa na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kupitia Chadema, Edward Lowassa na kuinanga serikali kuwa haijafanya lolote kwa miaka yote tangu uhuru.

Ingawa hakumtaja kwa jina, Dk. Magufuli alisema kuna mtu alikuwa na madaraka makubwa serikalini ambaye alidumu kwenye nafasi hiyo kwa miaka 10 lakini amekuwa akiilalamikia serikali aliyokuwa akiitumikia.

Sumaye alikuwa Waziri Mkuu katika serikali ya awamu ya tatu iliyokuwa ikiongozwa na Rais Benjamin Mkapa kwa kipindi cha miaka 10 mfulizo.

“Mtu alikuwa msaidizi wa karibu wa Rais na amekaa kwenye nafasi hiyo kwa miaka 10 mfululizo anasema hatujafanya kitu, ina maana yeye ndiye aliyetukwamisha akiwa madarakani,” alisema.
~Mpekuzi blog

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top