Featured

Loading...


Polisi Wakanusha Karatasi za Kura Zilizompa Alama Ya VEMA Magufuli Kukamatwa Masasi.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limekanusha taarifa zinazodaiwa kuandikwa katika mtandao mmoja wa kijamii, zikidai kukamatwa kwa baadhi ya watu katika kituo cha polisi wilaya ya Masasi mkoani hapa wakiwa na masanduku na fomu za kupigia kura zipatazo 2000 zikiwa tayari zimetumika.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Henry Mwaibambe, alisema taarifa hizo zilidai kuwa, fomu hizo zilimpa alama ya vema mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli na mgombea ubunge wa jimbo la Masasi kupitia chama hicho.

 Alisema taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa, mkuu wa wilaya ya Masasi aliingilia kati na watuhumiwa hao ambao hawakutajwa majina waliachiwa huru kwa dhamana kwa amri ya mkuu huyo wa wilaya ambaye ndiye aliewadhamini na kwamba masanduku hayo na karatasi yamehifadhiwa katika kituo cha polisi wilayani humo.
 
Kamanda Mwaibambe alisema taarifa hiyo ni uzushi na upotoshaji mkubwa na kwamba hakuna mtuhumiwa wala masanduku yaliyokamatwa mkoani hapa wala katika wilaya hiyo.

“Tunachofahamu kupitia kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (Nec), vifaa vya kupigia kura bado havijawasili nchini na alituahidi vitaanza kuwasili mwishoni mwa mwezi huu kutoka nchini Afrika Kusini.” alisema.

Alisema Jeshi la Polisi linamsaka mhalifu huyo wa mtandaoni na akitiwa mbaroni atafikishwa katika vyombo vya sheria.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top