Featured

Loading...


Makusanyo ya Halmashauri Nchini Yaongezeka kwa 800% Baada ya Kuanza Kutumia Mfumo wa Kielektroniki Kukusanya Mapato


Makusanyo ya mapato katika halmashauri nchini, yameongezeka kufikia asilimia 800 hadi 900 baada ya kuanza kutumika kwa mfumo wa kukusanya mapato kwa njia ya kielektroniki katika halmashauri 164.

Hayo yalibainishwa jana na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jaffo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma

Jaffo alisema Serikali imesanifu na kutengeneza mfumo wa kukusanya na kutoa ankara na hati za madai kwa kodi na tozo mbalimbali katika mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuachana na utaratibu wa kukusanya mapato kwa kutumia hati zinazoandikwa kwa mkono.

Alisema tangu halmashauri kuanza kutumia mfumo wa kukusanya mapato kwa njia ya kieletroniki, makusanyo yameongezeka kwa asilimia 800 hadi 900, hali ambayo inadhihirisha ukusanyaji mapato kwa njia ya stakabadhi za kuandikwa kwa mikono fedha nyingi zilikuwa zikipotea.

Alisema msingi wa kuanzishwa kwa matumizi ya mfumo huo ni kuanzisha matumizi ya benki ya TEHAMA katika kukusanya kodi na tozo mbalimbali na kuachana na utaratibu wa kukusanya mapato hayo kwa kutumia stakabadhi za kuandikwa kwa mkono, ambao hutengeneza mianya ya wizi na ubadhirifu wa fedha.

Alisema mfumo huo umekusudia kurahisisha utoaji wa stakabadhi na utunzaji kumbukumbu na kudhibiti upotevu wa mapato katika vyombo vinavyokusanya fedha za umma. 
Alisema serikali iliagiza ifikapo Julai 1, 2015, halmashauri zote ziwe zimeanza matumizi ya ukusanyaji wa mapato kwa mfumo wa kielektroniki, lakini ilipofika tarehe hiyo halmashauri 51 sawa na asilimia 28.18 ya halmashauri zote nchini, ndizo zilikuwa zimetekeleza agizo hilo.

Aidha, hadi mwanzoni mwa Desemba 2015 ni halmashauri 86 pekee sawa na asilimia 47.78 ndizo zilikuwa zimeingia katika hatua mbalimbali za utekelezaji wa agizo la serikali licha ya kupewa muda hadi Desemba 31, 2015.

Alisema kutokana na kusuasua kwa zoezi hilo la serikali, ndipo agizo la msisitizo lilitolewa na Ofisi ya Rais Tamisemi kuwa ifikapo Januari 10, mwaka huu halmashauri zote ziwe zimeingia katika mfumo huo; hivyo hadi Januari 12, halmashauri 164 sawa na asilimia 90.6 zimeingia katika hatua mbalimbali za ufungaji na matumizi ya mfumo.

Pia halmashauri 17 mpya sawa na asilimia 9.4, hazijaanza mchakato wa kufunga mfumo kwa sababu mbalimbali, zikiwemo kutokuwa na ofisi ya kudumu, kutofikiwa na Mkongo wa Taifa, umeme na zingine hazijagawana mali na halmashauri mama. Alizitaka zijipange kufunga mfumo huo.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright 2025 JICHO LETU | Designed By Code Nirvana
Back To Top