Featured

Loading...


MSD Yajiandaa Kuanza Kuzalisha Dawa Nchini


BOHARI Kuu ya Dawa (MSD), imesema iko kwenye hatua nzuri za kuanzisha mradi wa uzalishaji dawa na vifaa tiba nchini kwa ubia na sekta binafsi, lengo likiwa kupunguza tatizo la upatikanaji wa dawa na vifaa tiba nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Mwanakunu alisema zabuni ya kumpata mtaalamu mshauri imekwishatangazwa na inategemea kukamilika mwezi huu.

Alisema, kwa sasa Bohari huagiza kutoka nje ya nchi dawa na vifaa tiba takribani asilimia 80 kutokana na uchache na uwezo mdogo wa viwanda vya ndani vya kuzalisha dawa na vifaa tiba.

Bwanakunu alisema, hali hiyo huilazimu MSD kuagiza bidhaa zake kwa wingi kukidhi mahitaji ya muda mrefu na hivyo kulazimika kuwa na sehemu kubwa ya kuhifadhia bidhaa hizo.

Akizungumzia uwekaji nembo kwenye dawa za serikali, Bwanakunu alisema katika mwaka wa fedha 2013/ 2014, MSD ilianza kuweka nembo ya GOT ikimaanisha Government of Tanzania (Serikali ya Tanzania).

Alisema, nembo hiyo imewekwa kwenye vidonge, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara, kudhibiti kupelekwa kwenye maduka binafsi ya dawa, badala ya kutumiwa na walengwa ambao wanatibiwa katika hospitali zinazosambaziwa dawa na MSD.

“Awali, MSD ilikuwa ikiweka nembo ya MSD katika vifungashio tu, ambapo ilikuwa ni rahisi dawa hizo kuhujumiwa na kwenda kusikostahili. Kwa kuweka nembo hiyo ya GOT pamoja na MSD katika dawa, ni hatua mojawapo itakayosaidia kupunguza ama kudhibiti kabisa tatizo la wizi wa dawa za serikali,” Bwanakunu alisema.

Aliweka wazi kuwa hadi sasa asilimia 80 ya bidhaa zimekwishawekewa nembo ya GOT na kwamba wazabuni wengine wote wanaopata zabuni za kupeleka dawa kwenye bohari hiyo wanaelekezwa kuzingatia utaratibu huo wa kuweka nembo ya GOT na MSD.

“Kufikia Juni 2016 nembo ya MSD na GOT zitakuwa zimewekwa kwenye bidhaa zote,” alisema

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top