Featured

Loading...


Shirikisho la Wamiliki wa Shule Binafsi Waipongeza Serikali Kwa Kufuta Mfumo wa GPA na Kurudisha Division


Shirikisho la wamiliki wa shule na vyuo visivyo vya serikali  TAMONGSO watoa pongezi kwa Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi kwa kuliagiza Baraza la Taifa la Mitihani kufuta mfumo unaotumika sasa wa Wastani wa Alama (GPA) na kurudi katika mfumo uliokuwa unatumika hapo awali wa division.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti Taifa wa TAMONGSO Bwa. Mrinde Mzava amesema kuwa Waziri wa Elimu Ameitendea haki Sekta ya Elimu kwani mfumo huo ulileta sintofahamu kwa wananchi wengi.

“Waziri ameitendea haki sekta ya Elimu kwani mfumo wa GPA ulileta sintofahamu kwa wananchi na pia ulikuwa unaongeza ufaulu usio na mashiko kwa wanafunzi walio wengi ukilinganisha na mfumo uliokuwa unatumika awali,” aliongeza Mwenyekiti huyo.

Vilevile Mwenyekiti huyo alisema kuwa Tanzania inahitaji kuingia kwenye soko la upinzani hasa katika sekta ya Elimu  ili iweze kuajiri watu wenye utaalamu na sifa stahiki na kuweza kushindanishwa kwenye soko la kimataifa hivyo kwa mfumo wa GPA ulikuwa unadidimiza elimu ya Tanzania.

Mbali na hayo Mwenyekiti huyo alitoa agizo kwa baadhi wamiliki wa shule na vyuo visivyo vya Serikali kutotumia kigezo cha pesa ili kudidimiza kiwango cha Elimu nchini.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa shirikisho hilo Bwa. Emmanueli Gwegenyeza ameshauri viongozi na wananchi kwa ujumla kutochanganya suala la Siasa na Elimu kwani kwa kufanya hivyo tutazidi kudidimiza Sekta ya Elimu nchini.

“Tusiingize suala na Siasa na Elimu kwa wakati mmoja kwani kwa kufanya hivyo tunaweza kuididimiza Sekta ya Elimu pia tunaahidi kumpa Waziri ushirikiano ili kuzidi kuinua Sekta ya Elimu nchini,” aliongeza Makamu huyo.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top