Featured

Loading...


Waziri Muhongo aahidi kuongeza matumizi ya umeme wa makaa ya mawe


Serikali imesema itahakikisha makaa ya mawe yanakua chanzo kingine kikubwa cha uzalishaji wa umeme nchini ili kupunguza gharama za umeme zilizopo hivi sasa.

Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo ameyasema hayo  alipotembelea mgodi wa makaa ya mawe wa Ngaka uliopo wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma na kuongeza kuwa serikali itahakikisha inafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na mgodi huo ili kuimarisha uchumi wa taifa kupitia makaa ya mawe.

“Nimeelezwa makaa ya Ngaka yana  ubora na kiwango cha hali ya juu na nimeelezwa  kwamba kuna baadhi ya viwanda vimeingia mkataba na Ngaka lakini  badala yake wananunua makaa kutoka nje. Hilo halikubaliki ikiwa makaa ya ndani ya nchi yana ubora lazima tutumie bidhaa za nyumbani,”amesisitiza Prof. Muhongo.

Kutokana na malalamiko ya Mgodi kuhusu hali ya Mkataba ya kuuziana makaa kutoafikiana, Waziri Muhongo ameutaka mgodi huo,Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC),EWURA, Kampuni za Saruji za Dangote, Tanga Cement na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kukutana Makao Makuu ya Wizara tarehe 14 Januari,2016, ili kujadili  kuhusu suala hilo na pia kujadiliana juu ya  gharama za kuuziana umeme na TANESCO pindi mgodi huo utakapoanza kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Masoko wa mgodi wa Ngaka, Christopher Temba, mgodi huo unazalisha tani za makaa ya mawe laki tano kwa mwaka na tayari makaa hayo yanasafirishwa katika nchi za Kenya, Zambia, Malawi na vilevile katika viwanda kadhaa hapa nchini vikiwemo vya  Saruji, Mohamed Enterprises na viwanda vingine.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top