Featured

Loading...


FAMILIA KUFA AJALINI ‘KUNA MKONO WA MTU!'

Stori: Na mwandishi wetu
BADO ni kilio! Bado ni simanzi katika Kijiji cha Marangu, Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro kufuatia vifo vya wanafamilia watatu, Elimringi Minja, 60 (baba), Tudetsiwe Sanga, 48 (mke) na mtoto wao, Haikaeli John (10).
Watatu hao maisha yao yalikatishwa kwenye ajali ya Basi la Metro iliyotokea Septemba 15, mwaka huu katika eneo la Manga, Handeni mkoani Tanga na hivyo kuiacha nyumba yao katika ukimya wa maisha bila wao hata kama wataishi watu wengine.
Majeneza yakiandaliwa kwa ajili ya mazishi.
Kufuatia vifo hivyo, baadhi ya watu kijijini hapo walizungumzia maisha ya marehemu hao ya siku mbili kabla, hususan mke na mume huku wakionesha imani yao kwamba, kufa kwa watu hao kuna mkono wa mtu.
“Kama kweli binadamu tungepewa kuona kiroho, mzee Elimringi asingekufa. Siku mbili kabla ya tukio nilikutana naye, akasema alichofuata Dar kimekamilika, lakini anafikiria kusafiri Jumatano kurudi Moshi (Septemba 16) badala ya Septemba 15 siku ya Jumanne.
“Nilimuuliza kwa nini asiondoke Jumanne, akasema anaiona kama siyo siku ya safari. Lakini jioni yake akaniambia aliamua kusafiri Jumanne na familia yake na alishakata tiketi.
“Alisema kama kuna lolote baya acha litokee. Kumbe kweli baya lilikuwepo mbele yake. Ina maana aliliona kwenye ulimwengu wa kiroho. Binadamu tunatakiwa kusali sana, roho wa mauti anatuzunguka usiku na mchana. Lakini mimi naona kama kuna mkono wa mtu uliowamaliza wanafamilia hao. Ingawa maisha ya marehemu na familia yake hawakuwa na matatizo na watu,” alisema mzee Paschal, mkazi wa Dar aliyeshiriki mazishi hayo.
Mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la mama Jane akimzungumzia marehemu, Tudetsiwe alisema:
“Nalia mwanangu. Hapa si bure! Nalia bado kwa ajili ya kifo cha mama Haikaeli. Kinaniuma sana. mama Haikaeli mara ya mwisho nazungumza naye tulicheka sana, akasema tucheke kwa sababu kifo kipo na tukifa hatutaweza kucheka tena. Leo hii kweli yeye hawezi kucheka tena! Inauma sana.”
Majeruhi mmoja aliyelazwa Kituo cha Afya cha Mkata, Tanga alisema:
“Namshangaa sana Mungu mimi kuwa hai. Sina jema lolote lililomshawishi kunibakiza. Lakini ndani ya basi lile siku ile roho ya mauti ilitawala kwani tangu Dar abiria hatukuwa na mazungumzo mengi kama inavyokuaga ndani ya mabasi. Ukimya ulitawala. Ningejua nisingepanda lile basi.”
Marehemu Elimringi ambaye alikuwa Mwalimu Mkuu Shule ya Mbahe, Moshi Vijijini na familia yake walizikwa Septemba 18, mwaka huu kwenye kijiji hicho huku wachungaji na mapadri walishiriki kwenye ibada ya mazishi.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top