Featured

Loading...


Mgombea Urais wa TLP Asema Mrema Hajakosea Kumpigia Debe Magufuli


Mgombea urais kupitia chama cha TLP Macmillan Lyimo amesema anaunga mkono kauli ya mwenyekiti wake wa chama Mh. Augustine Mrema ya ‘kumpigia debe’ mgombea wa chama cha mapinduzi CCM, Dk John Magufuli, kwa madai kuwa hayo ni maamuzi yake binafsi.

Akizungumza na East Africa Radio mchana  huu, Lyimo amesema kuwa kauli hiyo haijatolewa na mkutano wowote wa chama, bali ni maoni binafsi kwa kuwa mwaka huu watanzania wanachagua mtu na siyo chama na kwamba jambo alilofanya Mrema si jipya wa la ajabu.

“Hili jambo siyo la ajabu, hata Marekani, Colin Powell alitangaza kumuunga mkono Obama licha ya kuwa chama tofauti, Mrema amesema hivyo kwa kuwa anajua looser siyo yeye, tumesimamisha wagombea ubunge nchi nzima, na yeye ni mmoja wapo, kwahiyo hilo halinipi shida” Amesema Macmillan Lyimo

Kuhusu mahusiano kati yake na mwenyekiti huyo, Lyimo amesema kuwa mahusiano ndani ya chama hicho ni mazuri na hakuna ugomvi wowote.

“Tunaendelea kushirikiana kama kawaida, na hata kampeni zangu nilianzia kwake na nitafungia jimboni kwake” kauli ya Lyimo

Kuhusu nafasi yake ya ushindi, Lyimo amesisitiza kuwa yeye ndiye atakayeshinda urais mwaka huu, na kamwe Rais hatoki CCM

“Magufuli hawezi kushinda, nafasi kubwa ya ushindi ninayo mimi, hata Magufuli anajua kuwa mimi napinga huo mwenge kwenye picha yake, hiyo ni ishara ya uchawi, na uchawi wake utashindwa mwaka huu”. Amesema mgombea huyo

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top