Featured

Loading...


Chopa ya CCM Yazua Kizaa zaa Mazishi ya Mtikila


Kada wa chama cha Mapinduzi ambaye pia ni mgombea ubunge wa jimbo la Ludewa mkoani Njombe jana aliwasili kwa chopa kwenye mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Siasa cha DP Mchungaji Christopher Mtikila.

Wakati chopa hiyo inatua katika eneo la Msiba wananchi waliacha kusikiliza Salam mbali mbali za viongozi na kukimbilia kutazama ili kufahamu ni nani aliyekuwemo ndipo alipoteremka Mgombea Ubunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe.

Mazishi ya Mchungaji Mtikila yalihudhuriwa na viongozi kadhaa wa serikalini akiwemo Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Mutungi, mkuu wa mkoa wa Njombe Dr. Rehema Nchimbi ,wanasiasa pamoja na ndugu na jamaa kutoka sehemu mbalimbali nchini Tanzania.

Akizungumza katika mazishi hayo Filikunjombe alisema mbali ya ukorofi wa Mtikila kwa kile alichokiamini ila kwake alikuwa ni mshauri mkubwa wa Ubunge wake katika jimbo la Ludewa.

Filikunjombe alisema katika kuamini kwake na kusimamia anachokiamini hadi umauti unamkuta alikuwa akitetea kuwepo kwa nchi ya Tanganyika na ndio maana kazikwa na bendera ya Tanganyika na kudai kuwa hakuna kosa kupigania Tanganyika kwani Tanganyika inahitajika.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dr. Rehema Nchimbi alisema kuwa Mkoa wa Njombe umepoteza kiongozi makini na kuwa katika kumuenzi ni vema kwa vyama vya siasa kuendesha kampeni za amani na utulivu  kuwa hivisasa taifa linaelekea katika uchaguzi mkuu.

Kwa upande mwingine Naibu Katibu mkuu wa DP Taifa Abdul Mluya alisema kuwa suala la kifo cha mwenyekiti wake ni utata mtupu na bado wanaendelea kuchunguza.
Filikunjombe akitoa salamu zake wakati wa mazishi ya Mtikila
Mkuu  wa mkoa wa Njombe Dr Rehema Nchimbi kulia akiwa na Deo Filikunjombe mgombea  ubunge jimbo la Ludewa na mbunge aliyemaliza muda  wake, katikati kushoto ni msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi jana  wakati wa mazishi ya Mchungaji Mtikila
Mjane  wa Mtikila  akiweka shada la maua

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top