Featured

Loading...


Mwalimu Apigwa Risasi Kichwani Kwa Kosa La Kujisaidia Haja Ndogo


POLISI wilayani Igunga mkoani Tabora inamshikilia mfanyabiashara kwa tuhuma za kumjeruhi kwa bastola mwalimu wa Shule ya Msingi Saint Leo.

Akizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Hamisi Selemani alisema tukio hilo ni la usiku wa Januari 15 mwaka huu katika baa ya Kibo iliyoko barabara ya Mwanzugi mjini Igunga.

Mganga Mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Igunga, Abdallah Ombeni amethibitisha kumpokea Mwalimu Theophano Mvula akiwa na jeraha kichwani ambapo alitibiwa kwa kushonwa nyuzi tatu na kuruhusiwa kwenda nyumbani. 
Kamanda Selemani alimtaja mwalimu aliyepigwa risasi kuwa ni Teophano Mvula mkazi wa mtaa wa Nkokoto kata ya Igunga.

Aidha kamanda huyo alisema chanzo cha kupigwa risasi mwalimu huyo ni kujisaidia haja ndogo jirani na gari la mfanyabiashara huyo, Felix Peter Mselel (42) mkazi wa Nzega.

Alibainisha kuwa baada ya kumuona mwalimu katika gari yake, aliamua kumfuata na baadaye yalitokea mabishano, hali iliyofanya mfanyabiashara kuchomoa bastola na kupiga risasi hewani huku risasi ya pili akimlenga kichwani mwalimu huyo.

Alisema baada ya kupigwa risasi mwalimu alianguka chini ambapo wasamaria walimchukua na kumkimbiza katika hospitali ya wilaya ya Igunga.

Hata hivyo, Kamanda Selemani alisema tayari mshitakiwa amekamatwa pamoja na bastola yake ikiwa na risasi 10 ambapo anategemewa kufikishwa mahakamani wakati wowote ili kujibu tuhuma inayomkabili.

Aidha Kamanda Selemani ametoa mwito kwa kamati zinazojadili na kupitisha majina ya watu wanaoomba kumiliki silaha kuwa makini, kwani bila kufanya hivyo inasababisha kupewa silaha watu wasiokuwa na sifa za kumiliki silaha jambo ambalo ni hatari.

Mwalimu Teophano Mvula akizungumza kutoka hospitali hapo, aliomba serikali kuwa makini na utoaji wa silaha kwa baadhi ya raia.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top