Featured

Loading...


Radi Yaua watu Watatu wa Familia moja Rufiji


Watu watatu wa familia moja, wakazi wa Kijiji cha Mchukwi wilayani hapa Mkoa wa Pwani, wamekufa baada ya kupigwa na radi jikoni wakati mvua zikinyesha.

Tukio hilo limetokea  jana jioni katika kijiji hicho. Inadaiwa kuwa radi hiyo ilianza kupiga mti uliokuwa pembezoni mwa jiko hilo kabla ya kuwaua ndugu hao.

Shuhuda wa tukio hilo, Amina Tenge ambaye pia ni Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho, alisema waliwachukua ndugu hao na kuwapeleka Hospitali ya Misheni ya Mchukwi kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya majeraha waliyopata.

“Tulipofika hospitali walikuwa wameshafariki tayari,” alisema Tenge.

Mganga wa zamu wa Hospital hiyo, Esther Mtini aliwataja marehemu hao kuwa ni Desteria Simba (40), Deborah Simba (2) na Amani Matimbwa (6).

Alisema baada ya kuifanyia uchunguzi miili hiyo, walibaini kuwa Desteria alikuwa ameungua kifuani, tumboni na shavuni.

“Amani aliungua tumboni na katika sehemu zake za siri na Deborah hakuwa na jeraha lolote,” alisema Dk Mtini.

Akizungumzia ajali hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Nurdin Babu aliwataka wananchi kuepuka kukaa chini ya miti au karibu na miti katika kipindi hiki ambacho mvua zinaendelea kunyesha kwani ni hatari kwa maisha yao.

“Mvua hizi zinazoendelea kunyesha sasa zina madhara kwa sababu zinaambatana na radi na upepo mkali, lazima tuchukue tahadhari kwa kuacha kukaa chini ya miti au jirani ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea,” alisema Babu.

Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), juzi ilitoa tahadhari ya kuwapo kwa mvua kubwa zinazoambatana na radi katika baadhi ya mikoa nchini, ukiwamo Pwani.    

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top