Featured

Loading...


Highnes Kiwia Kupinga Matokeo Ya Mabula Mahakamani

ALIYEKUWA mgombea ubunge Jimbo la Ilemela, Highnes Kiwia, kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ametangaza kwenda mahakamani kupinga matokeo yaliompa ushindi, Angelina Mabula (CCM).

Kiwia amesema kuwa matokeo yaliyompa ushindi Mabula yalikuwa ni ya kutengenezwa ili kumbeba mgombea huyo wa CCM kabla ya kufanyika kwa uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kiwia amesema atatumia haki ya kikatiba kupinga matokeo hayo mahakamani ili maoni ya wananchi kuheshimiwa na kupata haki zao za msingi.

Hata hivyo katika matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi huo, John Wanga, alimtangaza Angelina Mabula mshindi kwa kura 81, 424 dhidi ya Kiwia aliyepata kura 61,679.

Kiwia pia amesema kuwa katika baadhi ya vituo majina ya wapiga kura yaliongezwa, mawakala wake kutishiwa na baadhi ya wafuasi wa CCM kitendo ambacho dhahili alidai uchaguzi haukuwa huru.

“Kuna vituo ambavyo majina yaliongezwa, zaidi ya majina 700 ya wapiga kura yalihamishwa na kupelekwa Ukerewe, baada ya kupata taarifa ya kuhamishwa majina tulitoa taarifa kwa msimamizi wa uchaguzi lakini hatua hazikuchukuliwa.

“Matokeo haya yalikuwa yamepangwa kabla ya uchaguzi kufanyika, tunaenda mahakani kupinga matokeo haya, hatutaona maoni ya wananchi yanapotea,” amesema Kiwia.

Pia Kiwia alivitaja baadhi ya vituo ambavyo vilikuwa na kasoro kuwa ni pamoja na Kitangiri, Ilemela na Nyansaka na kwamba wamejipanga muda wowote kwenda mahakamani.

Kwa upande wake Kiongozi wa Chadema, Kanda ya Ziwa Victoria, Tungaraza Njugu amesema matokeo ya uchaguzi huo sio sahihi na kwamba maoni ya wananchi walio wengi yameporwa na CCM.
~Mpekuzi blog

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top