Featured

Loading...


Bodaboda Zinazopandisha ‘Mishikaki’ Kupigwa Picha


KATIKA kukabiliana na madereva wa pikipiki wanaopakia abiria zaidi ya mmoja maarufu mshikaki, Jeshi la Polisi mkoani Pwani litatumia mbinu mpya ya kuwapiga picha madereva hao na kuwakamata baadaye wakiwa kwenye vituo vyao.

Jeshi hilo litatumia mbinu hiyo ili kuepusha ukamataji kwa kuwakimbiza wale wanaofanya hivyo kwa lengo la kuepuka kusababisha ajali wakati wa kuwakamata madereva hao wanaobeba mshikaki.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Bonaventura Mushongi alisema kuwa mbinu hiyo itasaidia kuwabaini na kuwapiga faini kwa mujibu wa sheria.

“Tumeona tufanye hivyo kwani ukamataji wa zamani wa kufukuzana siyo mzuri, unaweza ukasababisha ajali kwa wanaotumia pikipiki hiyo na hata kugonga watu au mali katika kukwepa mkono wa sheria lakini kwa kuwapiga picha tutawatafuta na kuwakamata wakiwa hawana abiria,” alisema.

Alisema mbali ya kukamata madereva bodaboda wanaobeba mshikaki ambayo ni kinyume cha sheria, pia watawakamata kwa makosa mengine kama vile leseni, kutokuwa na kofia mbili ngumu na kutozingatia sheria za uendeshaji na usalama barabarani.

“Pia tunawaomba waendesha bodaboda watupe ushirikiano katika kubaini wahalifu ambao wamekuwa wakitumia usafiri huo kufanikisha wizi hivyo wanapaswa kutupa taarifa za watu wanaopanga kwenda kufanya uhalifu kutumia vyombo hivyo,” alisema Mushongi.

Aidha alisema kuwa endapo madereva hao wa bodaboda watatoa ushirikiano kwa polisi itasaidia sana kukabiliana na uhalifu ambao umekuwa ukijitokeza mara kwa mara.

“Pia kuna taarifa kuwa baadhi ya waendesha bodaboda nao wanajihusisha na uhalifu, tunawataka waache vitendo hivyo kwani wao ni watoa huduma na endapo watabainika kufanya hivyo watakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria,” alisema Mushongi.

Alibainisha kuwa jeshi lake litashirikiana na viongozi wa bodaboda katika kuhakikisha kuwa wanafuata sheria na kupambana na uhalifu na siyo wao kuwa chanzo cha uhalifu na kuvunja sheria.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top