Featured

Loading...


Ofisa TAKUKURU Auawa Kinyama.....Acharangwa Mapanga, Wauaji Watoweka


OFISA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) mkoani Dodoma, Emmanuel Meta (37) ameuawa kufuatia kupigwa na kukatwa mapanga  cha watu ambao mpaka sasa hawajafahamika.

Hata hivyo Jeshi la Polisi linamshikilia mtu mmoja kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo.

Tukio hilo lilitokea Januari 20, mwaka huu majira ya saa 6:15 usiku katika eneo la Area C manispaa ya Dodoma.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), David Mnyambuga, Ofisa huyo wa PCCB alifariki dunia wakati anapatiwa matibabu baada ya kupigwa na watu ambao hakuwafahamu.

Alisema mtoa taarifa wa awali wa tukio hilo, Athuman Mtengwa ambaye pia ni mfanyakazi PCCB, mkazi wa Area “D” alieleza kuwa, Januari 20, saa 6:15 usiku akiwa nyumbani kwake alipigiwa simu na Emmanuel (marehemu) ambaye ni mfanyakazi mwenzake pia ni rafiki yake wa karibu.

Alisema Meta alimweleza kuwa anaomba msaada wa kupelekwa hospitali kutibiwa kwa kuwa amepigwa na watu wasiofahamika wakati akirudi nyumbani kwake akitokea baa ya Rose Garden iliyopo Area “C” jirani na nyumbani kwake kwa matembezi.

Baada ya Mtengwa kufika alipiga honi ndipo Meta alitoka nje na kufunga mlango na geti kwa kufuli na kuingia katika gari kuelekea Hospitali ya Mkoa wa Dodoma na wakiwa njiani hali yake ilibadilika na kukosa nguvu na kushindwa kujimudu kwa lolote.

Alisema wakati akiendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Mkoa wa Dodoma alifariki dunia.

Kaimu Kamanda alisema uchunguzi wa mwili wa marehemu umefanyika ambapo amekutwa na jeraha kichwani linalovuja damu, alitokwa na damu puani na masikioni, uvimbe katika jicho la kulia na michubuko midogo mikononi.

“Mtu mmoja anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo unaendelea,” alisema Kaimu Kamanda.

Alitoa wito kwa mtu au watu wenye taarifa kuhusiana na tukio hili washirikiane na Jeshi la Polisi kuwafichua watu waliofanya uhalifu huo ili sheria ichukue mkondo wake.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright 2025 JICHO LETU | Designed By Code Nirvana
Back To Top