Featured

Loading...


Bunge laitaka Serikali kuharakisha ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeshauri Serikali kuharakisha ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha standard gauge ili kuisaidia Bandari ya Dar es salaam kukabiliana na ushindani kutoka bandari ya nchi jirani.

Hatua hii itasaidia kuleta maendeleo ya haraka hapa nchini kupitia upokeaji na usafirishaji wa  mizigo mingi ya nchini na nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Profesa Norman Sigala wakati akiwasilisha taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano ya mwaka ujao wa fedha.

Amesema kuwa nchi nyingine za wanachama wa Afrika Mashariki zinaendelea kujenga reli kwa kiwango cha standard gauge kutoka Mombasa kupitia Nairobi , Kampala hadi Kigali kwa kasi kubwa.

Mhe. Profesa Norman alisema kuwa ili Bandari za Tanzania ziweze kushindana na Bandari za Kenya katika kupokea mizigo ya nchi za Uganda na Rwanda ni vema reli ya kati ikajengwa kwa kiwango cha standard gauge ili iziunganishe nchi hizo na reli inawezesha kusafirisha mizigo bila vikwazo.

Aliongeza kuwa kukamilika kwa reli kwa kiwango hicho itasaidia kuwanufaisha mikoa 15 ya Tanzania bara.

Profesa Norman alisema kuwa ni vema Serikali ikaharakisha ujenzi wa reli ya kati na matawi yake yote ambayo ni kutoka Dar salaam kwenda kigoma, Uvinza hadi Msongati kwa ajili ya mizigo ya Burundi.

Alisema kuwa tawi jingine ni lile la kutoka Tabora hadi Kalemi kwa ajili ya mizigo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) na ile ya kutoka Tabora kupitia Shinyanga hadi Mwanza kwa ajili ya Ukanda wa ziwa.

Kwa upande wa Msemaji wa Kambi Rasmi  ya Upinzani Bungeni Mhe. James Mbatia akiwalisha maoni ya Kambi hiyo alisema kuwa reli ya kati ikiboreshwa itasaidia kutawala soko la usafirishaji wa abiria na mizigo ya ndani na nje ya nchi kama vile DRC, Burundi , Uganda na Rwanda.

Alisema kuwa hivi sasa watanzania wanatakiwa kuwa na reli ambayo itaendana na hali  ya sasa inayowezesha usafirishaji wa mizigo kwa kasi na uwezo mkubwa wa kubeba mzigo mzito.

Mhe. Mbatia alishauri kuwa ili kufupisha ujenzi wa reli hiyo ni vema kukawa na wakandarasi ambao watapewa vipande vidogo vidogo vya takribani kilometa 200 ambavyo vitajengwa kwa wakati.

Naye Waziri wa Ujenzi ,Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa alisema kuwa Serikali kupitia Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli(RAHACO) inaendelea na uboreshaji wa miundo mbinu ya reli ili kuongeza uwezo wa njia zilizopo za reli ya kati za kubeba mizigo mizito zaidi.

Alisema kuwa mara baada ya kukakamilisha uboreshaji wa reli hiyo kutasaidia uhimilivu wa  mwendo kasi wa juu na kupunguza ajali za treni.

Wizara hiyo imeliomba Bunge kuidhinisha shilingi 4,895,279,317,500.00 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali katika mwaka wa fedha ujao.

Kati ya fedha hizo shilingi 2,212,141,496,500.00 ni kwa ajili ya sekta ya ujenzi, shilingi 2,587,333,762,000.00 ni kwa ajili ya sekta ya uchukuzi na shilingi 95, 804,059,000.00 ni kwa ajili ya sekta ya mawasiliano.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top