Featured

Loading...


DARASA LA WAKUBWA TU: HIVI MAPENZI NI VITA?

WIKI iliyopita tulijadiliana kuhusu wapenzi wenye tabia ya kuwaacha wenzi wao na baadaye kulazimisha kuwarudia kwa nguvu na vitisho baada ya kugundua ndiyo wapenzi sahihi wa maisha yao.
Leo tunazungumzia mada inayosema, je, mapenzi ni vita? Ungana nami kujua mengi zaidi kupitia XXLove.
Nianze kwa kuwashukuru wasomaji wangu kwa kunitumia ujumbe mfupi wa ‘SMS’ na kunipigia simu, asanteni.
Kwenye mada ya leo ni dhahiri kuwa majibu ya haraka ya walio wengi ni lazima yatakuwa ndiyo au hapana na majibu hayo yako katika pande mbili kwa maana ya waliofurahia na walioumizwa kwa sababu ya mapenzi.
Hivi kweli mapenzi ni vita? Kama ni vita ya nani na nani? Na nini chanzo cha vita hiyo? Kama ni vita kwa nini watu bado wanajiingiza kwenye vita hiyo?
Kama hapana, mbona wengine wanauawa kisa mapenzi, kama unakataa mbona mama, baba, ndugu, rafiki au baadhi yetu hatuelewani na familia zetu kwa sababu ya mapenzi au uhusiano wako na fulani?
Wengine wanafungwa kwa sababu ya mapenzi na hata wengine wanajeruhiwa au kujeruhiana, kisa mapenzi. Ndugu na marafiki hawatembeleani kwa sababu ya ugomvi wa mapenzi.
Ukweli uko hivi; kuna wakati penzi huwa tamu sana kuzidi asali na wakati mwingine huwa chungu zaidi ya shubiri. Namaanisha hivi; kuna watu wengine wanafurahia uhusiano walio nao na wapenzi wao huku wengine wakionekana kujuta kwa nini hawakujuana mapema ili kufaidi raha hizo mapema.
Wakati huohuo, kuna wapenzi wengine wanajuta kuingia katika uhusiano na mpenzi huyo, yawezekana kwa kulazimishwa au yeye mwenyewe kupenda lakini leo anajuta. Anatamani aachike ili ajinasue lakini inakuwa ngumu.
Kwa wanaofurahia hawataona kuwa mapenzi ni vita lakini kwa walioumizwa, wataona ni vita kwa sababu yawezekana waliumizwa au wanaumizwa kila kukicha, wengi wanashindwa kuendelea na masomo yao, kisa kikiwa ni mapenzi, binti au kijana kashindwa au kafukuzwa nyumbani kwao chanzo kikiwa ni uhusiano na mtu fulani. Wengine wanafeli mitihani yao kwa sababu mpenzi wake kamchanganya.
Mara nyingi mpenzi msomaji, umekuwa ukisikia juu ya watu wanaolalamikia mapenzi kama chanzo cha kuharibika kwa maisha yao na mipango yao na kuyaona mapenzi kama vita. Ni vyema ukajua kuzungumza na moyo wako ili kufanya lililo sahihi kwenye uhusiano wako.
Tukutane wiki ijayo kwa somo lingine murua.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top