Featured

Loading...


Kilicho Mponza DIAMOND PLATNUMZ Tuzo za Kill Music Hichi Hapa, Wema na Jokate Watambiana Mabwana, Vanessa na Jux Wapakatana

Tuzo za Muziki za Kili 2015, Jumamosi ya wiki iliyopita zilitimua vumbi kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Mwenge jijini Dar es Salaam ambapo maelfu ya Watanzania wanaopenda burudani walikuwa wakifuatilia mwenendo mzima wa tuzo hizo, ambapo msanii Ali Kiba aling’ara baada ya kunyakua tuzo tano na kumuacha mbali hasimu wake mkubwa, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz’ aliyeambulia tuzo mbili tu.

Mpango mzima ulianza, mishale ya saa tatu za usiku ambapo wasanii pamoja na wadau mbalimbali walijumuika kwenye zulia jekundu na kupiga ‘mapichapicha’ ya ukumbusho kabla ya mchakato wa kutoa tuzo haujaanza.

Baada ya hapo, pazia la burudani lilifunguliwa na msanii chipukizi, Ruby anayetamba na ngoma yake ya Na Yule, akafuatiwa na Ommy Dimpoz, baadaye akapanda jukwaani Barnaba Elias sambamba na Vanessa Mdee, akapanda Christian Bella kisha Weusi wakiongozwa na Joh Makini na Nikki II wakafunga pazia la burudani kwa kukamua ile mbaya.

 ALI KIBA ANG’ARA

Ali Kiba.

Baadaye ulifuatia mchakato wa kutoa tuzo ambapo msanii Ali Kiba, alizoa tuzo tano; Mtumbuizaji Bora wa Mwaka, Wimbo Bora wa Mwaka (Mwana), Mtunzi Bora wa Mwaka (Bongo Fleva), Wimbo Bora wa Afro (Mwana) na Mwimbaji Bora wa Kiume (Bongo Fleva) huku hasimu wake Diamond Platinumz akiambulia tuzo mbili tu; Wimbo Bora wa Zouk/ Rhumba (Nitampata Wapi) na Video Bora ya Muziki ya Mwaka (MdogoMdogo).

 KILICHOMPONZA DIAMOND NI HIKI

Kutokana na matokeo hayo, inaelezwa kuwa kilichomponza msanii Diamond Platinumz ni ujumbe wake aliowahi kuutuma kwenye mitandao ya kijamii, akiziponda Tuzo za Kili kwamba hazizingatii vigezo, kwa kuwaacha wasanii wanaofanya vyema kwenye tasnia ya muziki na badala yake, ‘kuwapendelea’ baadhi ya wasanii kutokana na sababu binafsi za waandaaji.

“Unajua Diamond alikosea sana kuziponda Tuzo za Kili kwa sababu ndizo zilizompaisha mwaka jana, matokeo yake amempa nafasi mpinzani wake, Ali Kiba kung’ara kwa kunyakua tuzo kibao, nafikiri atakuwa amejifunza jambo,” alisema Bruno Sanga, mmoja kati ya wadau waliohudhuria utoaji wa tuzo hizo.

 WASHINDI WENGINE

Ukiachilia mbali Ali Kiba na Diamond, wengine walioziteka tuzo hizo ni mwanadada Vanesssa Mdee aliyenyakua tuzo mbili; Mtumbuizaji Bora wa Mwaka (Kike) na Mwimbaji Bora wa Kike (Bongo Fleva), Mzee Yusuph; Mwimbaji Bora wa Kiume Taarab, Mtunzi Bora wa Mwaka (Taarab) na Kundi Bora la Taarab (Jahazi).

Wengine ni Jose Mara aliyenyakua tuzo mbili, Isha Mashauzi, Joh Makini, Baraka Da Prince (Msanii Bora Chipukizi), Nahreel (Mtayarishaji Bora wa Mwaka) na Mrisho Mpoto aliyeondoka na Tuzo ya Wimbo Bora Wenye Vionjo vya Asili (Waite).

Sauti Sol walinyakua Tuzo ya Wimbo Bora wa Afrika Mashariki (Sura Yako), Profesa Jay (Wimbo Bora wa Hip Hop - Kipi Sijasikia), Jux (Wimbo Bora wa R&B- Sisikii) na Wimbo Bora wa Bendi wa Kiswahili iliyokwenda kwa FM Academia (Vijana wa Ngwasuma) na Bendi Bora ya Mwaka (FM Academia) huku Yamoto Band wakinyakua tuzo ya Kikundi Bora cha Mwaka (Bongo Fleva).
GPL

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top