Featured

Loading...


Urais 2015: January Makamba Apokelewa Kishujaa Mkoani Iringa, Apata Wadhamini 600


Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, ameungwa mkono na Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoani Iringa ambako alipata wadhamini zaidi ya 600. 
 
Akizungumza na wadhamini wake hao, January alisema endapo atafanikiwa kuwa rais atahakikisha CCM inalirudisha Jimbo la Iringa Mjini ambalo kwa sasa linaongozwa na Mchungaji Peter Msigwa kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwani ataweka kambi katika mji huo. 
 
Alisema kuwa ataimarisha miundombinu, ikiwa ni pamoja na kutanua kiwanja cha ndege cha Nduli na kukifanya kuwa cha kimataifa ili wananchi waweze kupata ajira kitakappingiza watalii wengi na kuongeza pato la mkoa huo pamoja na  kuzijenga barabara kwa kiwango cha lami. 
 
Aidha, January, alisema anaamini CCM kitamchagua kiongozi kwa kujiamini na kuwaomba wananchi wapuuze kauli za watu wanaodai kuwa endapo chama hakitawasimamisha katika  nafasi hiyo basi kitasambaratika. 
 
Alisema wananchi wanapaswa kutambua kuwa dhamana ya nchi hii iko mikononi mwa CCM, hivyo akipata nafasi hiyo au asipopata atakuwa mstari wa mbele katika kukirudisha chama pamoja kutokana na kuwa na makundi katika kipindi hiki cha uchaguzi. 
 
Aliongeza kwa kuwaomba wananchi wa mkoa huo kupitisha ushawishi kwa viongozi wanaopitisha majina kuwa wamchague kijana anayekusudia kuleta mabadiliko ya kweli ambaye ndiyo yeye. 
 
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Wenyeviti wa UVCCM mkoani humo, Kaunda Mwaipiana, alisema vijana hao wanamuunga mkono January katika kipindi chote kwani wanaamini anaweza kuivusha nchi hapa ilipo kutokana na hotuba yake nzuri aliyoitoa wakati akitangaza nia iliyobeba mikakati thatibi ya maendeleo. 
 
Naye Mwenyekiti wa Wilaya ya Iringa, Abeid Kiponza, alimpongeza kwa uthubutu wake wa kuomba nafasi hiyo na kwamba kama alivyoona vijana wenzake wa mkoa wa Iringa wameonesha nia ya kumuunga mkono.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top