Featured

Loading...


Wanaotangaza Nia ya Urais Wasichafuane na Kupakana Matope na Badala yake Wajipange Kuwaeleza Watanzania Jinsi ya Kuboresha Maisha Yao


Hakika Mungu ni mwema sana. Ametuwezesha leo kuwa na nguvu ya kutafakari hatima ya nchi yetu ambayo inaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 hapo Oktoba.
 
Mwishoni mwa wiki iliyopita tulishuhudia makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakijitokeza kuwania urais kupitia chama hicho na tayari wameanza kuchuana kutangaza nia yao baada ya vikao vya Kamati Kuu Taifa (CC) na Halmashauri Kuu Taifa (NEC) kumalizika hivi karibuni mjini Dodoma na kutoa baraka zote kuanza rasmi kwa mchakato huo.
 
Ninachowaomba watangaza nia ni kwamba wasitumie mwanya huo wa kujitangaza kuchafua wenzao na badala yake wajenge hoja bila kupitiliza kwa sababu kampeni rasmi zinazosimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi bado hazijaanza.
 
Kila mtangaza nia anatakiwa ajipange  kuwaeleza Watanzania jinsi ya kuboresha maisha duni ya wananchi kwani walio wengi ni magumu.
 
Watangaza nia wajipange kueleza jinsi ya kuondoa mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali nchini ambao uko  juu, wajipange kueleza wataisaidiaje jamii? 
  
Niwaase watangaza nia hasa kutoka chama tawala CCM kwamba kila neno watakalokuwa wanalitamka litakuwa linapimwa na wananchi.
 
Kwa hiyo basi, watangaza nia watakaotumia majukwaa kuwachafua wenzao, moja kwa moja watakuwa wamekwenda ‘nje ya reli’ kwa sababu sasa hivi wananchi wanataka kiongozi ambaye ataeleza jinsi ya kuwakwamuwa kiuchumi, kimatibabu na kielimu.
 
Ni jambo la msingi sasa kwa wana CCM kupima wagombea wao na wasijazane tu kwenye mikutano ya kutangaza nia na kushangilia kishabiki bila kupima neno kwa neno.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top