Featured

Loading...


WEMA SEPETU JIFUNZE KUWEKA BREKI MDOMONI


Wema Isaac Sepetu ‘Madam’
SALAMU nyingi zikufikie mrembo usiyechuja umaarufu tangu mwaka 2006, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ vipi uko poa? Mishemishe zinakwendaje?
Ukitaka kujua afya yangu, mimi namshukuru Mungu kwani ni mzima, hofu na mashaka ni kwako wewe uliye mbali na upeo wa macho yangu. Kitambo kidogo kimepita sijakuona lakini naamini u-mzima wa afya.
Mbali na kukusalimia, dhumuni la barua hii ni kutaka kukumbusha juu ya umuhimu wa mdomo wako kuwa na staha. Kuna vitu vya kuzungumza lakini kuna ambavyo vinapaswa kuwekwa ‘spea’.
Binafsi sikufurahishwa na namna ambavyo ulimpa maneno makali aliyekuwa rafiki yako, Kajala Masanja kupitia kipindi cha televisheni wiki iliyopita.Si busara kumtusi mwenzako hadharani kiasi kile. Hata kama amekukosea kiasi gani, wewe ni mtu maarufu unapaswa kuhakikisha kile unachokizungumza kitakuwa na matokeo gani mbele ya jamii inayokuzunguka.

Ugomvi wenu wewe na Kajala una historia ndefu, kibusara hakukuwa na sababu ya kuendeleza mjadala ambao hata watu tayari walishaanza kuusahau. Vitabu vya dini vinatufundisha, kusamehe na kusahau.

Nilishawahi kukuandikia barua huko nyuma, nilikusihi usamehe hili suala liishe. Nilisema hivyo kwa sababu mara kadhaa Kajala ameshaonesha nia ya kutaka yaishe lakini wewe ukaendeleza vita. Kwa nini usimsamehe? Mbaya zaidi hata huyo mwanaume ambaye inasemekana alikuibia naye nimetonywa kuwa ameshaachana naye.

Nyinyi mlishibana kama marafiki wa kuambiana kila kitu, la kwako la Kajala na la Kajala la kwako watu wanashindwa kuwaelewa kama kweli mlishibana kwa nini msikae na kuanza ukurasa mpya?

Sijawahi kumsikia Kajala anakuzungumzia vibaya lakini wewe kila siku unamsema. Unafikiri yeye hana mabaya yako? Akiyaanika hadharani utafurahi? Haiwezi kuwa sawa.Nakulaumu wewe zaidi katika hili maana historia inaonesha haudumu na marafiki. Uliwahi kuwa na urafiki na kina Jack wa Chuz, Rose Ndauka, Jamila na wengine kibao lakini wote uliwaacha njiani.

Kama hiyo haitoshi, Aunt naye mmedumu kwenye ushosti kwa muda mrefu lakini naye pia miezi kadhaa iliyopita mlitofautiana na sina hakika kama hadi sasa mpo sawa kama zamani japo mlipatanishwa.

Nikusihi, badilika. Kuwa na staha, chunga sana kauli zako kwani wewe unaheshimika katika jamii.
Nikushukuru kwa kunisoma!
Mimi ni kaka yako,
Erick Evarist 

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top