Featured

Loading...


Picha: Rais Magufuli Atua Jijini Arusha Kwa Kishindo......Aahidi Kuendelea Kutumbua Majipu Hadi Yaishe


RAIS John Magufuli ametoa mwito kwa Watanzania kumuombea ili aendelee kuwashughulikia wote wanaofanya ubadhirifu wa fedha za umma kupitia kampeni yake ya kutumbua majipu.

“Nataka niwahakikishieni kuwa nitaendelea kutumbua majipu yote mpaka yaishe, na naomba mniombee ili kazi hii ya kutumbua majipu ifanyike kwa mafanikio,” alisema Dk Magufuli.

Alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa akizungumza na wananchi katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha jana, alipotua kwa ziara ya kikazi ikiwa ni ya kwanza kwao tangu achaguliwe kushika wadhifa huo Novemba 5, mwaka jana.

Dk Magufuli aliwasili mkoani Arusha, ambako kesho atatunuku Kamisheni kwa maofisa wanafunzi wa kundi la 57/15 katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli mkoani hapa.

Rais Magufuli aliwasili mjini Arusha akitokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), alikotua kwa ndege akitokea jijini Dar es Salaam na kupokewa na mamia ya wananchi. 
Akiwa uwanjani hapo, Rais Magufuli aliwashukuru wananchi kwa mapokezi makubwa aliyoyapata na aliwaeleza kuwa uchaguzi umekwisha, kilichobaki ni kazi tu.

“Nawashukuru sana ndugu wananchi kwa mapokezi haya makubwa, naomba kuwahakikishia kuwa uchaguzi umekwisha na sasa kilichobaki ni kuchapa kazi tu,” alisema Rais Magufuli.

Alisema yote aliyoyaahidi kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na Watanzania kwa ujumla, ikiwemo ujenzi wa barabara za Arusha, kulipa fidia za wananchi na kufuta ada ya shule za msingi na sekondari yanatekelezwa.

Rais Magufuli alisisitiza kuwa serikali yake haitawabagua Watanzania kwa dini zao wala makabila yao na wala haitawabagua kwa misingi ya vyama vyao na kanda zao. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa KIA mkoani Kilimanjaro jana huku akiongozana na Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha Mhe.Daudi Felix Ntibenda tayari kwa hafla ya kuwatunuku kamisheni maafisa wapya wa jeshi la Wananchi waliohitimu vyema mafunzo yao katika chuo cha Jeshi Monduli Mkoani Arusha itakayofanyika Januari 23 /2016. PICHA NA IKULU
 Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akishiriki kupiga ngoma za utamaduni wakati alipowasili kwenye uwa nja wa ndege wa KIA mkoani Kilimanjaro jana
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi waliofika kumlaki kwenye uwanja wa ndege wa KIA mkoani Kilimanjaro.
Baadhi ya wananchi wakimpungia mikono Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa KIA mkoani Klimajaro.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright 2025 JICHO LETU | Designed By Code Nirvana
Back To Top