Featured

Loading...


ASKARI POLISI ANUSURIKA KUUAWA KWENYE MKUTANO WA CHADEMA BAADA YA KUFUMWA AKIREKODI

Mtia nia wa ubunge  Chadema jimbo la Geita Rodgers Luhega  akiwa anamuokoa  askari polisi aliyekuwa akipigwa na wananchi mara baada ya kuonekana anarekodi mkutano wao kwa kujificha.
Askari  wa  jeshi la Polisi  mkoani Geita  Insepekta  Zakayo amenusurika kuuawa baada ya kupokea  kipigo kikali kutoka kwa wananchi wenye hasira kali  kwenye mkutano wa  hadhara wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema uliofanyika mjini Geita  jana maeneo ya soko kuu la Geita.
 
Inaelezwa kuwa askari huyo ambaye alikuwa amevalia kiraia alifika katika mkutano huo akiwa na simu ambayo alionekana muda wote akirekodi kila kitu katika mkutano,na alikuwa akifanya hivyo kwa kificho.
 
Wakati akiendelea kurekodi mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Geita Alphonce Mawazo ,alipanda jukwaani na kumuona akiendelea kurekodi....akasema
 
"Maaskari tunawaheshimu sana ,tunajua kwamba kuna baadhi mnaagizwa na wakubwa zenu kuja kurekodi vitu ambavyo tunavizungumza ,sisi hatukatai mtu kurekodi,kama unataka kurekodi kwanini usije sehemu ya wazi unafanya kwa kificho “alisema.
 
Kuna askari ambaye tunamfahamu kavaa kiraia na helmenti nyekundu na yupo hapa anarekodi......"

 
Baada ya kusema hayo wananchi walimvamia askari huyo na kuanza kumpiga ngumi  maeneo mbalimbali ya mwili wake hali ambayo ilisababisha askari huyo kupata majeraha usoni  na mkutano kuvurukika kwa muda wa dakika 5.
 
Aidha baada ya  wananchi kumvamia Askari huyo Mawazo aliagiza walinzi wa chama  hicho maarufu kama  Red Briged kuwazuia  wananchi wasiendelee kumpiga huku akiwataka wananchi hao waache kumpiga Askari.
 
Hata hivyo wananchi hao hawakusikia ndipo Askari wanchadema walipoamua kutumia nguvu kwa kuwatawanya wananchi na kufanikiwa kumuokoa.


 
"Makanda mwacheni,msimpige makamanda, Red Briged kamuokoeni huyo “alisema mawazo ambapo askari hao walienda kumuokoa na muda mfupi gari ya jeshi la polisi ikiwa na askari  wa  kikosi cha kutuliza ghasia na kumpakiza kisha  kwenda kituoni naye kituoni wakiwa na makamanda wa Chadema",alisema
 
Kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Peter Kakamba alikili kutokea kwa tukio hilo na  kwamba uchunguzi bado unaendelea wa kubaini waliofanya tukio hilo.
 
“Ni kweli kuna Askari wetu amepigwa,lakini tunaendelea na uchunguzi wa kuwatafuta watu waliomshambulia askari huyo na nitatolea ufafunizi kesho saaa 4:00 asubuhi".
 
Hata hivyo baada ya vurugu hizo kuisha mkutano huo  uliolenga kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye Daftari la wapiga kura linalotarajia kuanza Juni 9 mwaka huu mkoani humo uliendelea ,ambapo Mawazo  alimlalamikia  Mkurugenzi wa Halmasahuri ya mji Margareth Nakainga kwa kuweka vituo vichache vya kujiandikisha na kudai hali hiyo ni njama za CCM .
 
“Inashangaza mji wa Katoro ulivyo mkubwa na watu wengi, lakini wameweka kituo kimoja cha kujiandikisha,hii inaonyesha  wengi hawatajiandikisha kwani wengi watatembea umbali mrefu zaidi ya km 8,na walivyowajanja maeneo mengi ambayo chadema imeshinda  uchaguzi wa serikali za mitaa ndiko wamepeleka vituo vichache”alisema Mawazo.
 
Pia alitoa angalizo kwa tume ya uaNdikishaji kuwa makini kutatua tatizo hilo mapema  ili yasitokea machafuko kwani wananchi hawatakubali  kuona wenzao wanandikishwa na wengine kuachwa na kwamba  utaungana nao  kufanya maandamano makubwa yasiyo kuwa na kikomo ili kupinga hujuma hizo.
 
Aidha katioka mkutano huo baadhi ya watia nia wa kiti cha ubunge na udiwani jimbo la Geita mjini  walijitokeza  rasmi na kutanga za nia yao ya kugombea nafasi hizo  katika jimbo  hilo ambapo nafasi ya ubunge walijitokeza  saba na   udiwani zaidi ya 10 na kuwaomba wananchi kuwaunga mkono ili kulikomboa jimbo hilo.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top