Featured

Loading...


WAKUBWA TU: FANYA HIVI KUMPATA ANAYEKUFAA-2

Karibu katika muendelezo wa mada yetu tuliyoanza wiki iliyopita, mada yetu inajieleza hapo juu.Tulijifunza wiki iliyopita kabla ya kutafuta atakayekufaa na kukupenda, wewe binafsi unapaswa kufanya yafuatayo;
Jiepushe na makundi
Umri wa kijana ndiyo pekee wenye changamoto nyingi sana katika uso wa dunia kama vile ; vishawaishi, tamaa, majaribu na mengineyo. Kama kijana unapaswa uchague watu wa kuwa nao usipende kufuata mkumbo kwa sababu John au Juma wanafanya kitu flani basi na wewe unaiga. Tabia ya kuiga ni kukosa kujiamini kama kijana, jaribu kuwa wa kitofauti, siyo kila kitu huigwa, vingine hupuuzwa pia.
Jichunguze
Unapaswa ujichunguze kwa makini, wewe ni wa thamani kiasi gani? Na mwisho ujue wewe si wa kila mtu anayetaka kupumzika na kujistarehesha basi anapumzikia kwako.
Jiheshimu
Lazima ujiheshimu kwanza wewe na wengine watakuheshimu tu bila kujali kipato, elimu au jinsia yako, lakini kama utakuwa waluwalu kila mtu akikutaka anakupata, asipite msichana yeyote mbele yako unaye hilo ni tatizo.
Jitathmini
Je, ni vitu gani vitamfanya mwanamke au mwanaume aweze kuwa mwenza wako, je ni tabia yako nzuri au mbaya? Ni tabia yako ya roho mbaya au upendo? Uzinzi na uongo au uchoyo na ushirikina?
Sababu zote nilizoorodhesha hapo juu, haziwezekani kufanyika ipasavyo kama hutakuwa mtu wa kufanya maombi. Kwani katika maombi utamuomba Mungu akupe mke au mume mwema. Katika maombi utaomba Mungu akujalie hekima, busara, adabu na upendo kwa mke au mume atakaye kuzawadia.
Bidii katika maombi    
Swala la ibada ni jambo muhimu sana kwenye maisha ya mwanadamu, kila muda na kila mahali, si tu mpaka wakati wa matatizo. Vijana wengi wa Kikiristo wamesahau kuwa ‘Kumcha Mungu ndiyo chanzo cha maarifa,’ mke mwema anatoka kwa Mungu, hata vijana wa Kiislam nao wamesahau kuwa ‘Allah akbar ‘(Mungu mkubwa).
Kama vijana watatumia nguvu, akili na muda wao mwingi katika kumtukuza Mungu kwa sala, kufunga na maombi inawezekana kukupa mtu anayefaa kama mumeo au mkeo.

Tukutane wiki ijayo katika mada nyingine nzuri.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top