Featured

Loading...


CHUO CHA KAMPALA INTERNATIONA UNIVERSITY CHAFUNGWA KISA MGOMO WA WANACHUO

Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala(KIU)

Mgomo wa wanafunzi wa vitivo vya Sayansi ya Afya vya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala(KIU)- tawi la Dar es Salaam, umesababisha chuo hicho kufungwa.

Mgomo huo uliokwenda sambamba na maandamano ya wanafunzi, ulisababisha Polisi kuingilia kati na kupambana na wanafunzi hao na baadaye uongozi wa chuo kikifunga kwa muda usiojulikana.
 
Wanafunzi hao waligoma kufanya mitihani kutokana na uongozi wa chuo kushindwa kushughulikia usajili wa kozi za famasia, maabara na udaktari.  
 
Mmoja wa wanafunzi wa shahada ya udaktari mwaka wa pili, alisema wameamua kugomea mitihani kutokana na kutojua hatma ya kozi wanayosoma kama imesajiliwa hivyo kuushinikiza uongozi kuhakikisha kozi hizo zinafanyiwa usajili.
 
“Uongozi umekuwa ukitupa ahadi ya kushughulikia madai yetu kwa muda mrefu, cha kushangaza hadi sasa hakuna majibu ya kuridhisha juu ya usajili wa kozi zetu,” alisema.
 
Aidha, alisema uongozi wa chuo umeshindwa kuwatatulia matatizo hali inayosababisha migomo isiyokwisha.
 
Naye, mwanafunzi wa Shahada ya Famasia mwaka wa pili, alisema tangu Baraza la Famasia liwape siku 10 kusajili kozi hadi leo kozi yao haijafanyiwa usajili. 
 
Rais wa KIU, Elias Mbogho, alisema wanafunzi wachache wa kozi ya Famasia ndiyo wanawashawishi wenzao kugomea mitihani akisisitiza usaili wa kozi hiyo umefikia katika hatua nzuri.
 
“Mgomo unaofanyika hauwahusishi wanafunzi wote wa vitivo vya Sayansi ya Afya, bali wanafunzi wa famasia wanachochea mgomo,” alisema.
 
Kwa mujibu wa Afisa Masoko na Mahusiano wa chuo hicho, Kenneth Uki, kutokana mgomo huo wanafunzi wanne walijeruhiwa na kutibiwa katika zahanati ya KIU kufuatia  vurugu zilizozuka juzi chuoni hapo.   
 
Uki, alisema mgomo huo ulisababisha uharibifu wa milango minne na madirisha 75 ambayo hadi sasa thamani yake  haijajulikana.
 
Alisema wanafunzi wanane walikamatwa na polisi na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Stakishari-Ukonga.
 
Aliongeza kuwa uongozi wa KIU umelazimika kufunga vitivo vya masomo ya sayansi kwa muda usiojulikana.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top