Featured

Loading...


MKURUGENZI WA WIZARA YA AFYA KORTINI KWA TUHUMA ZA RUSHWA


Mkurugenzi wa Afya na Usafi wa Mazingira wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Elias Chinamo akipelekwa rumande chini ya ulinzi wa polisi kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam jana. Chinamo anatuhumiwa  kwa kosa la kuomba na kupokea rushwa. 
Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Afya na Usafi wa Mazingira wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Elias Chinamo amefikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu akikabiliwa na mashtaka 14 ya kuomba na kupokea rushwa.
Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leonard Swai alidai wakati akisoma mashtaka jana mbele ya Hakimu Mkazi Renatus Rutta, kuwa mshtakiwa huyo alitenda makosa hayo kati ya Juni 2011 na Februari 2013.
Swai alidai kuwa katika kipindi hicho mshtakiwa aliomba na kupokea rushwa ya zaidi ya Sh14.44 milioni.
Mwendesha Mashtaka huyo alidai kuwa Chinamo alipokea rushwa ya Sh6.1 milioni kutoka kwa Suzana Nchala, fedha ambazo alidai alizipokea kupitia akaunti yake yenye namba 0152237197600 iliyopo tawi la benki ya CRDB la Holland.
Alidai kuwa alipokea fedha hizo kama faida ya kumpa nafasi ya kuandaa semina mbalimbali na mikutano ya wizara hiyo, kitu ambacho kipo kinyume na matakwa ya mwajiri wake.
Pia mwendesha mashtaka huyo alidai kuwa Chinamo alipokea Sh2.06 milioni kutoka kwa Fadhili Kilemile, fedha ambazo zilipitishiwa kwenye akaunti hiyo kwa lengo la kumpa nafasi ya kuandaa semina mbalimbali na mikutano ya wizara hiyo kinyume na matakwa ya mwajiri wake.
Katika shtaka jingine, Chinamo anadaiwa kupokea Sh3.28 milioni kutoka kwa Emmanuela Safari, Sh700,000 kutoka kwa Joseph Bilango na Sh2.3 milioni kutoka kwa Anyitike Mwakitalima kupitia akaunti ya CRDB na 019201018063 ya NBC, tawi la Kichwele.
Chinamo aliyakana mashtaka hayo na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wake umekamilika.
Hakimu Rutta alimuachia huru mshtakiwa huyo baada ya kukamilisha masharti ya kusaini dhamana ya Sh10 milioni pamoja na kuwa na wadhamini wawili waliosaini hati ya dhamana ya maneno yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha. Kesi imeahirishwa hadi Julai Mosi, 2015 atakaposomewa maelezo ya awali.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top