Featured

Loading...


Rais Kikwete Kuvunja Bunge July 9


Hatimaye imebainika kwamba Bunge la 10 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, litafikia ukomo wake Julai 9, mwaka huu.

Hadi kufikia mwisho wa uhai wake, Bunge hilo lililoongozwa na Spika Anne Makinda (pichani),  na Naibu Spika Job Ndugai, litakuwa limefanya mikutano 20  huku vikao vya mwisho vikiwa ni 38.

Ratiba ya nyongeza iliyotolewa jana na ofisi ya Bunge baada ya kikao cha Kamati ya Uongozi, ilionyesha kuwa Rais Jakaya Kikwete atalivunja Bunge hilo baada ya kulihutubia.

Pamoja na tukio hilo la kihistoria, Bunge limejadili miswada mbalimbali ikiwamo (iliyopitishwa) ya sheria ya fedha ya mwaka 2015, sheria ya vituo vya pamoja mipakani ya mwaka 2015 na sheria ya kufuta sheria ya benki ya Posta ya mwaka 2015.

Aidha, baada ya maoni ya wadau wa habari, muswada wa haki ya kupata habari ambao ulikuwa ujadiliwe Juni 27, mwaka huu, baada ya kusomwa kwa mara ya kwanza, uliondolewa bungeni hadi serikali ijayo.

Miswada inayoendelea kujadiliwa ni muswada wa sheria ya masoko ya bidhaa wa mwaka 2015, muswada wa sheria ya kuwalinda watoa taarifa za uhalifu na mashahidi wa mwaka 2015.

Mingine ni muswada wa sheria ya Petroli wa mwaka 2015, muswada wa sheria ya usimamizi wa mapato ya mafuta na gesi wa mwaka 20q5, muswada wa sheria ya uwazi na uwajibikaji katika tasnia ya uchimbaji Tanzania ya mwaka 2015.

Ratiba hiyo imeonyesha kuwa muswada mwingine ni wa sheria ya Tume ya walimu wa mwaka 2015.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top