Featured

Loading...


Hatma ya Kesi ya Kukaa Mita 200 Baada Ya Kupiga Kura Kutolewa Leo


MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo itatoa uamuzi kuhusu shauri la kikatiba lililofunguliwa na Mbunge wa Viti Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Amy Kibatala likihoji uhalali wa wapigakura kukaa mita 200 kutoka kwenye vituo vya kupigia kura.

Mwenyekiti wa Jopo la Majaji watatu linalosikiliza kesi hiyo, Sekieti Kihiyo alisema Dar es Salaam jana wakati akiahirisha kesi hiyo iliyotajwa kwa ajili ya maelekezo muhimu alisema, uamuzi huo utatolewa saa 4:00 asubuhi. Pamoja na Jaji Kihiyo, majaji wengine wa kesi hiyo ni Lugano Mwandamba na Aloycius Mujulizi.

Kesi hiyo ilitajwa jana kwa ajili ya maelekezo muhimu. Kesi hiyo imefunguliwa na Amy anayegombea ubunge Viti Maalumu Jimbo la Kilombero, Morogoro, dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC).

Amy anaiomba Mahakama itoe tafsiri ya Kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Uchaguzi Sura ya 343 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2010, kinachohusu uhalali wa wananchi kukaa meta 200 kutoka katika kituo cha kupiga kura.

Kesi hiyo ilianza kusikilizwa juzi ambapo Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Tulia Ackson akisaidiwa na jopo la mawakili wanane, aliiomba Mahakama itupilie mbali kesi hiyo kwa kuwa kifungu cha sheria kilichotumika siyo sahihi na pia mlalamikaji hajaeleza jinsi gani haki yake itakiukwa.

Alidai sheria ambayo ilitakiwa kutumika ni ya Matumizi ya Sheria na siyo ya Utekelezaji wa haki za msingi. Pia alidai kifungu wanachoomba kitafsiriwe, kinakataza mikutano ya aina yoyote bila kujali umbali wa kituo cha kupigia kura au cha kuhesabia kura.

Isemavyo sheria ya uchaguzi

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top