Featured

Loading...


Kikwete: "Kutumia Fedha Nyingi Kujenga Jeshi Letu siyo Ubadhirifu wa Fedha"


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa Tanzania inaimarisha Jeshi lake – Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), siyo kwa nia ya kumchokoza mtu ama nchi yoyote, bali kwa nia ya kulinda mipaka yake kwa sababu kila hatua ya maendeleo ina changamoto tofauti za ulinzi wa nchi.

Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa siyo uharibifu kutumia fedha nyingi kujenga Jeshi, kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wanadai, kwa sababu ni wajibu wa kila nchi kuhakikisha kuwa Jeshi lake linakuwa katika utayari wa kukabiliana na uchokozi wa aina yoyote.

Rais vile vile amesema kuwa uchumi wa Tanzania, na hasa uchumi mpya wa gesiasilia, ambayo ndiyo itakuwa msingi mkuu wa uchumi na maendeleo ya Tanzania lazima ulindwe kwa njia yoyote na kwa nguvu zote.

Rais Kikwete aliyasema hayo Jumatatu, Oktoba 19, 2015 wakati alipozungumza katika Sherehe ya Kukamilisha Mradi wa Ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa Kurushia Ndegevita na Sherehe ya Kufungua Mradi wa Kuongeza Urefu wa Uwanja wa Ndegevita katika Kituo cha Kijeshi cha Kamandi ya Anga cha Ngerengere, Mkoa wa Morogoro.

Rais aliwaambia walioshuhudia sherehe hiyo akiwemo Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China katika Tanzania Mheshimiwa Dkt. Lu Youquing kuwa Tanzania inajenga Jeshi lake vizuri kwa ajili ya ulinzi wa mipaka yake.

“Hatujengi Jeshi letu kwa nia ya kumchokoza yeyote ama nchi yoyote. Tunajenga Jeshi letu kwa nia ya kulinda mipaka yetu. Na kweli huwezi kujua, katika dunia yetu hii wakorofi na wachokozi wapo. Kwa sasa hawapo lakini huwezi kusema kuwa hawatakuwepo milele. Inawezakana mtu akaamua kutuchokoza na hivyo lazima tuwe tayari kulinda mipaka yetu. Iddi Amin alikurupuka hivyo hivyo.”

Rais kikwete aliongeza: “Na wala tusije kujidanganya. Kutumia fedha nyingi kujenga Jeshi letu siyo ubadhirifu wa fedha. Ni jambo la lazima kabisa. Ni matarajio yangu kuwa sera za namna hiyo zitaendelea, hata chini ya uongozi ujao, hata kama baadhi ya watu wanaweza hata wakaanza kufikiria sera ya kupunguza matumizi ya kijeshi….yatakuwa ni makosa makubwa.”

Rais Kikwete pia ameishukuru nchi ya Jamhuri ya Watu wa China kwa kuisaidia Tanzania katika masuala ya ulinzi, akisisitiza kuwa katika ujenzi wa Jeshi la Tanzania hakuna nchi rafiki kama China duniani. “Ni wajibu wetu kuwajua na kuwashukuru marafiki zetu wa kweli.”

China ndio inagharimia miradi hiyo miwili ya maboresho ya Uwanja wa ndegevita wa Ngerengere ambao ukikamilika utakuwa na uwezo wa kuhudumia hata ndege kubwa za abiria ikitokea hali ya dharura katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wa Dar es Salaam.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
21 Oktoba, 2015
~Mpekuzi blog

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top