Featured

Loading...


UKAWA Wasitisha Kampeni Ngazi Zote


VYAMA vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimesitisha kampeni zake ngazi zote ili kutoa fursa kwa wananchi kuaga mwili wa aliyekuwa mwenyekiti mwenza, Dk. Emmanuel Makaidi.

Dk. Makaidi, aliyekuwa pia Mwenyekiti wa National League for Democracy (NLD) alichokianzisha mwaka 1992, na mgombea ubunge jimbo la Masasi mkoani Mtwara, alifariki dunia Alhamisi wiki iliyopita katika hospitali ya Nyangao, Masasi, baada ya kuugua ghafla ugonjwa wa shinikizo la damu (presha).

Ofisa Habari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tumaini Makene, akizungumza kwa niaba ya UKAWA, jana jijini Dar es Salaam, alisema usitishaji wa kampeni umelenga kuonesha heshima ya kipekee kwa Dk. Makaidi ambaye alijitoa muhanga katika kuimarisha UKAWA kwa hali na mali.

“Kesho (Leo) kuanzia saa tatu asubuhi tutakuwa viwanja vya Karimjee kwaajili ya kutoa heshima za mwisho kwa Dk. Makaidi, sambamba na hilo pia tutasitisha kampeni zetu za ngazi zote na katika shughuli hiyo viongozi wote wa kitaifa wa UKAWA pamoja mgombea Urais watakuwepo” alisema Makene.

Baada ya mwili wa Dk. Makaidi kuagwa katika viwanja vya Karimjee, shughuli ya mazishi ya mwanasiasa huyo mkongwe aliyefariki akiwa na umri wa miaka 74 itahitimishwa katika makaburi ya Sinza jijini Dar es Salaam.

Ratiba ya kampeni itaendelea Jumatano ya tarehe 21 Oktoba kwa mgombea urais wa Ukawa, Edward Lowassa kwenda mkoani Morogoro kumalizia majimbo ambayo hakufika katika awamu yake ya kwanza ya kampeni mkoani hapo.

Majimbo hayo ni pamoja na jimbo la Kilombero, Mlimba, Mikumi, Ulanga Mashariki na Ulanga Magharibi.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top