Featured

Loading...


Chadema Kupinga Ushindi wa Hussein Bashe Mahakamani


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilaya ya Nzega mkoani Tabora kimetangaza kwenda mahakamani kupinga matokeo yaliyompatia ushindi Mbunge wa jimbo la Nzega Mjini, Hussein Bashe (CCM).
 
Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Nzega, Hawa Mniga alimtangaza Hussein Bashe kuwa mshindi baada ya kupata kura 18,774 akifuatiwa na mgombea wa Chadema, Charles Mabula aliyepata kura 9,658.
 
Akizungumza katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa kwa kuwashukuru wananchi kwa kukipigia kura chama hicho, Mwenyekiti wa jimbo hilo Mabula alisema uchaguzi huo haukuwa huru na haki kutokana na kasoro nyingi kujitokeza na baadhi ya vituo kuwa na zaidi ya karatasi tatu za matokeo.
 
Alisema rushwa ilitawala siku ya kupiga kura ikiwa na vurugu licha ya kuripotiwa katika mamlaka husika hakuna jitihada zilizochukuliwa.
 
Alisema kwa sasa wanasheria wanaendelea na mikakati ya kuandaa kesi na muda wowote shauri hilo litafunguliwa katika Mahakama Kuu ya Kanda ya Tabora ili haki iweze kutendeka na kila mgombea apate kura halali alizopigiwa na wananchi.
 
“Uchaguzi huu haukuwa huru na haki rushwa zilitolewa sana,vurugu na udanganyifu mkubwa katika vituo mbalimbali hivyo tunaona sasa njia mbadala ya kupata haki zetu ni mahakamani na hapa sitoweza kusema hoja zote hapa lakini ushahidi umekamilika na muda wowote tutapanda mahakamani,” alisema.
 
Mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya Nzega, Omary Omary ambaye ni Diwani wa kata ya Bukene aliwataka wananchi kuwa watulivu katika kipindi hicho wakati chama hicho kinapinga matokeo ya ubunge mahakamani.
 
Alisema kuwa uchaguzi huo uligubikwa na kasoro nyingi ambazo zitaweza kutatuliwa na Mahakama na kuongeza kuwa wananchi wanapaswa kuendelea na shuguli zao za maendeleo ikiwa na kudumisha amani na utulivu.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top