Featured

Loading...


Chadema ‘Wajigamba’ Kufawafanyisha Polisi Maandamano


Katika hali isiyo kuwa ya kawaida Chama cha Demokrasia na Maendeleo mkoani Shinyanga leo kimedai kwamba Jeshi la Polisi mkoani humo limefanya maandamano ya Chadema bila kujijua.

Kwa mujibu wa baadhi ya viongozi wa chama hicho walidai kupokea taarifa kutoka kwa uongozi wa juu wa chama hicho ukiwataka kufanya maandamano leo nchi nzima  ya kupinga ushindi wa Dkt. John Pombe Magufuli kwa madai kuwa demokrasia imebakwa katika mchakato mzima wa uchaguzi  mkuu uliofanyika tarehe 25 oktoba 2015.

Katibu wa Chadema wilaya ya Shinyanga mjini George Kitalama amesema kwamba chama hicho kimefanikiwa kufanya maandamano kupitia  jeshi la polisi lililozunguka mji mzima kuwasaka wanachama wa chadema na kuambulia patupu.

“Tulipanga kufanya maandamano leo Novemba 03,2015 mji mzima wa Shinyanga lakini polisi ndiyo wamejitokeza kufanya maandamano wakiwa na magari yao kila mtaa.”Alisema Kitalama.

Kufuatia taarifa  ya Chadema kutaka  kufanya maandamano katika maeneo mbalimbali nchini Askari wa Jeshi la Polisi wamekuwa  katika misururu ya magari yakiwemo ya maji ya kuwasha wakizunguka kuwasaka waandamanaji kutoka chama hicho ambao hawakufanikiwa kufanya maandamano hayo.

Jijini Dares salaam Askari Polisi wakiwa kwenye punda na wengine wa doria wameonekana katika maeneo mbalimbali ikiwemo maeneo nyeti na yenye ofisi nyingi za Serikali ikiwemo Posta.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top