Featured

Loading...


Lowassa Kuongea na Watanzania Leo jijini Arusha


Aliyekuwa mgombea wa urais wa Chadema, Edward Lowassa anatarajia kuhutubia mkutano wa kumnadi mgombea wa ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema na kuwashukuru Watanzania kwa kura walizompa katika Uchaguzi Mkuu uliopita.

Jeshi la Polisi limeridhia mkutano huo utakaofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Ngarenaro, lakini limepiga marufuku maandamano yoyote.

Huu utakuwa mkutano wa kwanza wa hadhara kwa Lowassa tangu matokeo ya uchaguzi mkuu yalipotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ambayo yalimpa ushindi mgombea wa CCM, Dk John Magufuli. Lowassa alipata kura 6,072,848, sawa na asilimia 39.97 wakati mshindi Dk Magufuli alijikusanyia kura 8,882,935 sawa na asilimia 58.46

“Tunatarajia kesho (leo) aliyekuwa mgombea wa urais wa Chadema chini ya mwavuli wa Ukawa, Edward Lowassa atahutubia mkutano wa kampeni wa kawaida akiongozana na viongozi wengine wa kitaifa,” alisema Katibu wa Chadema Wilaya ya Arusha, Lewis Kopwe, alipozungumzia kukamilika kwa maandalizi yote ya mkutano huo jana.

Kopwe alisema mkutano huo ni sehemu ya mikutano ya kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arusha Mjini na amehimiza amani na utulivu vitamalaki katika mkutano huo.

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas jana alisema wamepiga marufuku maandamano ya aina yoyote katika mikutano ya kampeni inayoendelea.

Alionya Jeshi la Polisi halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote ambaye ataandamana na kusababisha kuvunjika kwa amani katika Jiji la Arusha. “Kuna watu, kwa maslahi yao, wanataka kutuvunjia amani, sasa tunaonya tutachukua hatua kali kwa yeyote ambaye atavunja sharia,” alisema Kamanda Sabas.

Pamoja na onyo hilo, alisema kuwa hadi jana jeshi hilo, lilikuwa halijapata barua yoyote ya kutaka maandamano na hata ikiwapo hawatakuwa tayari kuruhusu yafanyike. Pia, alisema jeshi hilo liko vizuri na limejipanga kuhakikisha amani na utulivu vinadumu kama ilivyokuwa wakati wa Uchaguzi Mkuu Oktoba 25 mwaka huu.

Katika hali inayoonyesha kwamba Jeshi la Polisi halitanii, jana jiji la Arusha lilikumbwa na taharuki kutokana na magari makubwa ya kurusha maji ya kuwashwa kupitishwa mitaani huku yakiwa kwenye mwendo kasi.

Kamanda Sabas alisema kilichokuwa kinafanyika ni mazoezi ya kawaida ambayo yanathibitisha kuwa polisi ipo imara. “Haya ni mazoezi ya kawaida, tunajua uchaguzi bado unaendelea na tumejipanga kulinda amani ya Arusha,” alisema.

Lema, ambaye anajiandaa kutetea kiti hicho alisema kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni kwamba Lowassa atazungumza leo na Watanzania, pia kuwashukuru kwa kumpigia kura nyingi.

Naye Mbunge mteule wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi “Sugu” alisema katika mkutano huo Chadema watatoa tamko zito la kwanza mara baada ya uchaguzi huo wa madiwani, wabunge na rais kumalizika.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top