Featured

Loading...


Sakata Dk. Mwaka Lawa Pasua Kichwa kwa Dk. Kigwangalla

 
Utata kuhusiana na uhalali wa tiba zinazotolewa na Dk. Juma Mwaka wa kituo cha tiba mbadala cha Foreplan Clinic kilichopo Ilala jijini Dar es Salaam unaelekea kuwa ‘pasua kichwa’ kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dk. Hamis Kigwangalla, baada ya majibu ya uchunguzi wa vyeti vya mganga huyo kushindwa kutolewa kwa umma kama ilivyoahidiwa.

Awali, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wiki iliyopita, Waziri Kigwangalla aliahidi kutoa taarifa kwa umma kuhusiana na Dk. Mwaka juzi (Jumatatu). Alieleza hayo baada ya kufanya ziara ya ghafla kwenye kituo cha Dk. Mwaka Desemba 14, 2015 na kutomkuta yeye na baadhi ya watoa huduma wake kabla ya kumtaka (Dk. Mwaka) awasilishe vyeti vyake wizarani kwa ajili ya ukaguzi.


Hata hivyo, licha ya Dk. Mwaka kutekeleza agizo alilopewa Desemba 16 na waziri kukiri kuwa kweli vyeti hivyo vimefikishwa kwao na kuhakikiwa, bado suala lake linaelekea kusumbua kwani hadi kufikia jana, hakukuwa na ufafanuzi zaidi kama ilivyoahidiwa wiki iliyopita huku Dk. Kigwangalla akiutaka umma utulie na kusubiri taarifa ya ukaguzi kwani hivi sasa kuna masuala mengine ya kushughulikia.

 “Tutawapa taarifa mara tutakapomaliza kuipitia ripoti hiyo, subirini tu kwa kuwa kuna kazi nyingi za kufanya wizarani,” Dk. Kigwangalla wakati alipoulizwa na mwandishi wa Nipashe jana kuhusiana na matokeo ya ukaguzi wa vyeti mwaka kama alivyoahidi wiki iliyopita.

Akieleza zaidi, Dk. Kigwangalla alisema bado anaipitia ripoti hiyo na akishamaliza, atashauriana na viongozi wengine wa wizara yao akiwamo Waziri mwenye dhamana, Ummy Mwalimu, na kisha ndipo ataitisha mkutano na waandishi wa habari kwa ajili ya kutoa taarifa.

ILIVYOKUWA
Desemba 14 ya wiki iliyopita, Dk. Kigwangalla alifanya ziara ya kustukiza kwenye kituo cha Dk. Mwaka ambaye amekuwa maarufu kutokana na matangazo mbalimbali anayotoa kila mara kuhusiana na tiba anazotoa.

Hata hivyo, baada ya Dk. Kigwangalla kufika kwenye kituo hicho, hakumkuta Dk. Mwaka na wenzake na ndipo (Dk. Kigwangalla) alipotoa amri ya kufungwa kwa muda kituo hicho akimtuhumu Dk. Mwaka na wenzake kumkimbia na kisha akaamuru apeleke vyeti vyake ili vichunguzwe na kuona kama huduma wanazotoa zinakidhi vigezo na ni salama kwa wagonjwa.

Desemba 20, Kigwangalla aliiambia Nipashe kuwa ameshapokea ripoti yenye maelezo ya vyeti vya Dk. Mwaka na kwamba, angetoa ufafanuzi kwa vyombo vya habari Jumatatu au Jumanne (juzi au jana).

chanzo; http://www.udakuspecially.com/2015/12/sakata-dk-mwaka-lawa-pasua-kichwa-kwa.html

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top