Featured

Loading...


Waziri Kitwanga Aanza Ziara Zake Kwa Kutembelea Jeshi La Polisi......Awapa Polisi Siku MOJA Ya Kujieleza ni Kwa nini Hawalindi Bandari Ya Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga ametoa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza ni kwa nini askari hawalindi Bandari ya Dar es Salaam badala yake kazi hiyo inafanywa na kampuni binafsi za ulinzi.

Kitwanga amepanga kukutana na viongozi waandamizi wa Polisi kesho ili kujadili mipango na mikakati mbalimbali ya kuongeza ufanisi wa kazi ya kuwahudumia wananchi.

Akizungumza na maofisa waandamizi wa polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam baada ya kufanya ziara katika Chuo cha Taaluma ya Polisi na kuangalia makazi ya askari, Kurasini, Kitwanga alieleza kusikitishwa na hatua ya polisi kuacha kutoa ulinzi bandarini na kuita kitendo hicho kuwa ni udhaifu wa jeshi hilo.

Alisema kitendo hicho kimetoa mwanya kwa baadhi ya wafanyabiashara kukwepa kodi wakati wa kushusha bidhaa zao akisema Bandari ni eneo la mpaka ambalo linahitaji ulinzi wa polisi kama mipaka mingine ya nchi.

Akionekana kukerwa, Waziri Kitwanga alimkatisha Kamishna wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipojaribu kutoa sababu akimtaka kutumia siku nzima ya leo kuandaa majibu ili kesho wayazungumze kwenye kikao rasmi. 
 
Waziri Kitwanga amelitaka pia jeshi la polisi kumweleza mipango ya kukabiliana na dawa za kulevya kwa sababu ndiyo zimekuwa chanzo cha matukio mengi ya uhalifu ikiwamo tishio la ugaidi.

Alisema haiwezekani kitengo cha kupambana na dawa za kulevya kikaachiwa jukumu hilo wakati jeshi la polisi liko kwenye operesheni zake kila siku.

Kuhusu msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam, waziri huyo alisema ni uzembe wa askari wa usalama barabarani kwa sababu wameshindwa kusimamia sheria na kuwachukulia hatua madereva wazembe.

Alisema zipo nchi za Afrika ambazo hazina askari wa barabarani kwa sababu kiwango cha nidhamu ya madereva wake ni kikubwa na wamekuwa wakifanya vizuri kuhakikisha kwamba suala la msongamano usio wa lazima unadhibitiwa kwa kufuata sheria.

Baadhi ya askari walimweleza Kitwanga kero zao. Mmoja wao, Alphonce Malowa alisema nyumba za askari ni chache na nyingi zimechakaa kiasi cha kuwafanya kudharaulika mbele ya wananchi.

Inspekta Novatus Makondowa alieleza juu ya umuhimu wa Serikali kuwasomesha walimu wa chuo cha taaluma za polisi ili kuwajengea uwezo zaidi wa kufundisha maofisa wengine chuoni hapo.     
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati) akitoka kuikagua moja ya nyumba ya zamani ya Jeshi ya Polisi ambayo inakaliwa na baadhi ya askari iliyopo Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil. Waziri Kitwanga alizikagua nyumba hizo za zamani pamoja na zakisasa zilizopo katika eneo hilo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia) akiiangalia nyumba ya mabati ya makazi ya Polisi wakati alipoingia ndani huku akitokwa na jasho kutokana na joto kali ndani ya nyumba hiyo. Waziri Kitwanga alifanya ziara ya kutembelea nyumba hizo zilizopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Katikati ni Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, na kushoto ni  mkazi wa nyumba hiyo, ambaye ni askari Polisi, Nelson Chale.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top