Featured

Loading...


Hamad Rashid: Serikali ya Muungano isibabaishwe na wahisani


Mjumbe wa Kuteuliwa wa Baraza la Wawakilishi, Hamad Rashid (ADC) ametaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutobabaishwa na nchi washirika wa maendeleo kwa kususa misaada yao kwa kile alichosema, nafasi ipo ya kutumia rasilimali ziliopo kikamilifu.

Rashid, ambaye alikuwa mgombea wa nafasi ya urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ADC katika uchaguzi wa marudio, alisema hayo wakati akichangia hotuba ya rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein aliyoitoa katika uzinduzi wa baraza la wawakilishi.

Mwakilishi huyo alionya nchi hizo akitaka zisitumie uwezo wao kwa ajili ya kulazimisha matakwa yao na kupinda sheria za nchi zinazotokana na demokrasia iliopo.

Alisema Tanzania bado inao uwezo mkubwa wa kutumia rasilimali zake zinazotokana na utajiri mkubwa kwa ajili ya kujenga nchi na kupambana na umasikini lakini viongozi walikuwa wakibweteka kutokana na kuwepo kwa misaada ya nchi matajiri.

“Tusibabaishwe na wahisani kwa tishio lao la kusitisha misaada ya maendeleo...wakati umefika wa kufanya kazi na kutumia rasilimali zetu kikamilifu ikiwemo kukusanya mapato na kupambana na viongozi wazembe na wabadhirifu."

Rashid mwanasiasa mkongwe ambaye aliwahi kuwa naibu waziri wa fedha na uchumi wa Serikali ya Muungano katika miaka ya 1987, alisema huu ni wakati wa kuiga mfano wa nchi ya Kenya wahisani walizuia misaada kwa asilimia 80 lakini walitumia walichonacho kwa ajili ya matumizi ya ndani.

Mapema Rashid alimpongeza Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohmed Shein kwa kumteua kuwa mwakilishi, hatua ambayo imetimiza ndoto zake za kuunda serikali itakayovishirikisha vyama vya siasa nchini kinyume ma matarajio ya wapinzani.

“Hii siyo serikali ya umoja wa kitaifa lakini ni serikali iliyowajumuisha wananchi na vyama vyote vya siasa na sasa tupo tayari kufanya kazi kwa ajili ya kuleta na kusimamia maendeleo kwa faida ya wananchi wote kwa sababu uchaguzi umekwisha,’’alisema.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top