Mwandishi wetu
Mambo ya uchaguzi! Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibroad Slaa wamezua jambo baada ya kusababisha mpasuko miongoni mwa wanachama wa chama hicho.
Mambo ya uchaguzi! Mgombea Urais wa Chadema, Edward Lowassa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibroad Slaa wamezua jambo baada ya kusababisha mpasuko miongoni mwa wanachama wa chama hicho.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika ofisi za makao makuu ya chama hicho, Kinondoni, Dar wakati wa zoezi la uchukuaji wa fomu za kuwania nafasi hiyo, baadhi ya wanachama hao walionekana kutofautiana juu ya nani hasa kati ya wanasiasa hao wawili alistahili kusimamishwa.
“Lowassa angekaribishwa na kuwa mwanachama wa kawaida tu, hii nafasi ilistahili kuchukuliwa na Dk. Slaa kwa sababu siku zote tunamuamini kama kiongozi makini na mwenye maono,” alisema mwanachama mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Komu.
Lakini wanachama wengine walioonekana kumuunga mkono Lowassa, walisema kutompa nafasi hiyo ya kugombea urais kada huyo kutoka CCM, ni kupoteza bure nafasi iliyokuja bila kutarajiwa, kwani waziri mkuu huyo wa zamani ana wafuasi wengi kutoka ndani ya chama tawala na kuwa wataongeza mno idadi ya kura za ushindi.
“Hii ndiyo nafasi ambayo Chadema ilikuwa inaisubiri kwa miaka yote, wote tumeona jinsi alivyokuwa na wafuasi wengi ndani ya CCM, kutompa agombee urais ni kujikosesha ushindi makusudi, tuna imani na Lowassa,” alisema.
Tangu kukaribishwa kwa Lowassa ndani ya Chadema, chama hicho kikuu cha upinzani kimekuwa na mgawanyiko mkubwa, hasa kwa kile kinachodaiwa kususa kwa Dk. Slaa ambaye aliyejijengea umaarufu mkubwa kutokana na misimamo isiyoyumba.
Post a Comment