Featured

Loading...


Kauli ya UKAWA Kususia Uchaguzi Yaishtua NEC.


Tume  ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imeshtushwa na kauli  iliyotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kwamba watasusia uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Hata hivyo, Nec imetetea kauli iliyotolewa  na Mjumbe wa Kamati ya Kampeni ya Mgombea urais  ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo, kwamba CCM haitakubali kuiachia Ikulu Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva, alisema kauli hiyo iliyotolewa na kiongozi wa chama kikubwa iliwashtua na kwamba katika vipindi vyote vya uchaguzi vilivyopita, hawajawahi kukumbana nayo.
 
Hata hivyo, Jaji Lubuva alisema baada Nec kufuatilia, ilibaini  kuwa kilichosemwa na Bulembo, hakiendani na kauli  iliyotolewa na Mbowe. 

Jaji Lubuva alisema kauli iliyotolewa na Mbowe si tu kwamba inashtua, lakini  ni hatari kutolewa katika kipindi hiki muhimu cha uchaguzi ambacho Watanzania na nchi nyingine,  zinaamini kwamba uchaguzi utafanyika katika hali ya amani na utulivu. 
 
Lakini alisema baada ya kufuatilia, wamebaini kuwa kauli iliyotolewa na Bulembo katika mkutano wa kampeni za CCM mjini Kigoma ilikuwa ni ya kisiasa na si vinginevyo.

“Bulembo katika kauli yake hajasema kwamba hata kama Nec ikitangaza matokeo CCM wakiwa wameshindwa,  hawatakuwa tayari kuwaachia Ikulu Chadema. Alikuwa anamaanisha kuwa watawashawishi wapiga kura wao wasiwapigie kura ili wasipate nafasi ya kwenda Ikulu,” alisema. 
 
Alisema  kauli iliyotolewa na Mbowe na Bulembo zinakinzana na kwamba baada ya kufuatilia walizinukuu.

“Kukataa matokeo ya uchaguzi hata kama umeshindwa kihalali ni uhaini,” alisema Jani Lubuva.

“Hii ni kauli ya kisiasa kama ambavyo Chadema nao wamekuwa wakitamka kwamba hii ndiyo awamu ya mwisho kwa CCM kukaa madarakani,” alisema Lubuva.

Kadhalika, Jaji Lubuva alikemea na kulaani kauli mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na wagombea, viongozi  wa vyama vya siasa na makada wake katika kampeni zinazoendelea kote nchini.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top