Featured

Loading...


Lowassa: Nitaunda tume kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji


Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema kupitia mwamvuli wa Ukawa, Edward Lowassa amesema kuwa ataunda tume ya maridhiano itakayoshughulika migogoro ya wakulima na wafugaji ili kuondokana na matatizo ambayo yamekuwa yakiwasumbua.

Lowassa amesema tume hiyo ndiyo itakayokuwa mwarobaini wa matatizo ya wakulima na wafugaji nchini ambao wamekuwa wakipigana na kuleteana matatizo ambayo yamechukua muda kutatuliwa.

Mgombea huyo amesema hayo yatawezekana pale tu atakapochaguliwa kuingia madarakani katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Akizungumza jana na wananchi wa Matui ambao wengi wao ni wakulima na wafugaji katika uwanja wa Soweto wilayani Kiteto Lowassa alisema tume hiyo itapitia matatizo yote ya wakulima na wafugaji na kutoa suluhisho la uhakika.

“Serikali yangu itapitia migogoro hiyo na kulipa fidia zinazostahili kwa wale walioathirika na migogoro iliyoibua mapigano kati ya wakulima na wafugaji katika maeneo mbalimbali nchini,”alisema Lowassa huku akishangiliwa na wananchi hao.

Alisema wakishalipa fidia hizo na kutatua migogoro hiyo matatizo kati ya wakulima na wafugaji hayatajirudia tena.

Katika Wilaya ya Kiteto kumekuwa na mgogoro wa wakulima na wafugaji ambao umekuwa ukizungumzwa katika Bunge la 10 ukihusishwa pia na wakazi wa Wilaya ya Kongwa.

Lowassa alisema kuwa serikali yake itapima ardhi yote nchini ili kutambua maeneo ya wakulima na wafugaji ili wasiweze kuingiliana na kuleteana shida.

Kwa upande wake aliyekuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole Medeye alisema Lowassa akiingia madarakani matatizo ya wakulima na wafugaji yatatatuliwa ndani ya miezi miwili nchini kote.

Ole Medeye alisema kuwa Waziri Mkuu ameshindwa kutatua migogoro ya ardhi nchini na badala yake amekuwa akitalii tu katika maeneo hayo badala ya kusikiliza matatizo ya wananchi.

~Mpekuzi blog

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top