Featured

Loading...


MAMA DIAMOND AMKARIBISHA WEMA

Brighton Masalu 
MAMBO yamekuwa mambo! Siku chache baada ya mzazi mwenza wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kutimka Bongo na kuelekea kwake nchini Afrika Kusini ‘Sauz’, mama mzazi wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ ameibuka na kusema hana kinyongo na mpenzi wa zamani wa mwanaye, Wema Sepetu ‘Madam’ na anamkaribisha nyumbani kwao muda wowote, Risasi Jumamosi lina ‘full’ stori.
Wema Sepetu ‘Madam’ akiwa na mama mzazi wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’.
Tangu Zari aondoke Bongo, imeelezwa kuwa, familia ya Diamond chini ya mama huyo mzaa chema, imempotezea ‘mazima’ Zari na endapo Wema ataamua kurudi nyumbani, atapokelewa kwa mikono miwili.
MWANAFAMILIA AVUJISHA UBUYU
Mmoja wa wanafamilia wa Diamond ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, mwishoni mwa wiki iliyopita, kwa zaidi ya dakika 34, alizungumza na mwanahabari wetu na kudai kutokana na ‘gepu’ lililoachwa na Zari, kuna uwezekano mkubwa Wema akarudisha majeshi kwa Diamond na mambo yakawa kama zamani kwani hana kipingamizi.
“Unajua Zari hawezi kurudi, mtu pekee ambaye tuna imani naye na tuliishi naye vizuri ni Wema, yaani hata kama ni kumshawishi, tutafanya hivyo ili arudi kwenye kiti chake kilichokaliwa na Zari kwa muda.

Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na aliyekuwa mpenzi wake Wema Sepetu.
MAMA DIAMOND SASA
Baada ya kuzipata habari hizo, mwandishi wetu alimtafuta mama Diamond kwa njia ya simu, ambapo baada ya kuulizwa juu ya madai hayo, awali mama huyo ambaye hapo zamani alisifika kwa ustaarabu na upole, ‘alifyatuka’ kwa maneno makali na kumtaka mwanahabari wetu kutofuatilia maisha ya familia yake.
“Kwani, bila familia yangu huwezi kufanya kazi zako? Mbona hivyo lakini? Au na wewe uje kuishi huku basi kama unaona sisi tunafaidi,” alibwatuka mama Diamond.
AMKUBALI WEMA, AMKARIBISHA NYUMBANI
Baada ya mwandishi wetu kumbana mama huyo na kumtaka arudi kwenye hoja ya msingi ya kuzungumzia aliyekuwa mchumba wa mwanaye (Wema), bi mkubwa huyo alisema hana kinyongo naye na anamkaribisha nyumbani kwa Diamond, Madale-Tegeta, Dar (anapoishi pia mama huyo) muda wowote kuanzia sasa na yuko tayari kuona akiwa karibu na mwanaye, Diamond.
“Sijawahi kugombana na Wema, ni wao tu walishindwana kidogo katika mapenzi yao. Lakini mimi namkaribisha hata leo. Hapa ni kama kwake. Ni binti mwema na furaha yangu ni kumuona akiwa karibu na mwanangu hata kama ni maisha ya kawaida tu,” alisema mama Diamond na kukata simu kabla ya kuizima kabisa (mwandishi alimtafuta tena).
WEMA ANASEMAJE?
Awali jitihada za kumpata Wema ili aweze kuzungumza kama yupo tayari kurudisha moyo wake nyuma na kurejea kwenye himaya ya Diamond hazikuzaa matunda kufuatia mrembo huyo kuwa bize na kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) na simu yake kutopokelewa.
Hata hivyo, muda mfupi kabla ya kwenda mitamboni, Wema alipatikana ambapo alitoa la moyoni juu ya ishu hiyo:
“Siwezi kurudia kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume kutoka familia ya Kiswahili.”
KUMBUKUMBU MUHIMU
Mara kadhaa, Wema alishawahi kuulizwa kupitia magazeti tofauti Pendwa ya Global Publishers (Ijumaa Wikienda, Uwazi, Ijumaa ‘Kubwa’, Amani, Risasi Jumatano, Risasi Jumamosi) kama anaweza kurudiana na Diamond, akadai hayupo tayari hata iweje!

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top