Featured

Loading...


NEC: Kalamu Yoyote inaruhusiwa Kupigia Kura


Ili kuondoa shaka miongoni mwa wananchi kutokana na tetesi zinazosambazwa juu ya ubora wa kalamu za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kila mtu anaruhusiwa kuja na kalamu yake kupigia kura Oktoba 25, mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa leo na NEC wakati ilipofanya mkutano wake na wahariri wa vyombo vya habari nchini ikiwa ni siku ya tatu ya kukamilisha utaratibu wa kuzungumza na wadau wa uchaguzi baada ya kufanya hivyo kwa wawakilishi wa walemavu na wamiliki wa vyombo vya habari nchini.

Akisisitiza juu ya ushiriki wa wadau kutoa elimu ya mpiga kura, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Lubuva amesema kipindi hiki cha kampeni kimeshuhudia kuzuka kwa maneno mengi yasiyokuwa na uhakika ambayo yanawachanganya wananchi.

“Kalamu yoyote inaruhusiwa kupigia kura hivyo watu wasiogope kwenda na kalamu zao ila wasiokuwa nazo watatumia zetu tulizoziandaa. Hazifutiki kama inavyosemwa huko mitaani,” amesema Jaji Lubuva.

Ametumia nafasi hiyo pia kubainisha mkakati wa kuzuia uwezekano wowote wa wizi wa kura kama inavyosemwa na baadhi ya wagombea na viongozi wa vyama vya siasa na kutoa wito kwa mtu au taasisi yoyote inayoona mwanya wa hilo kujitokeza ili hatua stahiki zichukuliwe.

Vile vile amewataka wanasiasa wote kuachana na maneno machafu wawapo majukwaani pamoja na kushambulia tume hiyo au baina ya wenyewe kwa wenyewe na badala yake wajikite kwenye kunadi sera zao.

“Tunaumizwa sana na matumizi ya maneno kama ‘tume inaandaa bao la mkono’ kwenye vyombo vyenu. Hakutakuwa na wizi na sisi tunaamini ushindi utatokana na wingi wa kura alizopata mgombea husika,” amesema na kuongeza:

“Kama chama cha siasa kimeishiwa sera za kunadi kwa wananchi basi ni vyema kikampumzisha mgombea wake na kusubiri siku ya uchaguzi badala ya kutoa lugha zisizofaa. Matumizi ya kauli za matusi, dhihaka au kejeli dhihi ya wagombea wengine ni kinyume na maadili ya uchaguzi. Hata kuituhumu tume bila kutoa ushahidi siyo jambo jema na kutowatendea haki wananchi.”

Mwenyekiti huyo ametoa kauli hizo baada ya kupata michango kutoka kwa wahariri waliomueleza changamoto walizonazo katika kuruhusu matumizi ya baadhi ya maneno yanayotolewa majukwaani.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top