Featured

Loading...


Dk. Magufuli Afuta Hatimiliki Shamba la Mkonge Kikwetu

Serikali imefuta hatimiliki ya shamba la mkonge la Kikwetu, mkoani Lindi baada ya mmiliki wake kampuni ya Amboni Estates Ltd, kushindwa kuliendeleza.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wakazi wa manispaa hiyo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Ilulu mjini hapa juzi.


Shamba hilo linalodaiwa kupewa hati ya umiliki wa miaka 99 na baadaye kampuni ya Tasco kabla ya kuchukuliwa na Mohamed Enterprieses Tanzania Ltd lilikuwa likizalisha mkonge kwa ajili ya kutengeneza magunia na bidhaa zingine.

Akizungumza katika mkutano huo, Waziri  Mkuu Majaliwa alisema kupitia mamlaka aliyopewa kisheria, Rais Magufuli  amefuta leseni ya umiliki wa shamba hilo na kuwa chini ya serikali.

Majaliwa alisema tayari shamba hilo lipo huru na kampuni ya BSG ipo huru kujenga mitambo itakayotumika kusafishia gesi asilia kwenye eneo hilo.

Kuhusu uendelezwaji wa kiwanda cha kuzalisha saruji cha Meis ambacho ujenzi wake umesimama kwa muda kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za kisiasa, Majaliwa alisema kazi hiyo inatarajiwa kuanza tena muda mfupi ujao baada ya kupatikana kwa wataalam.

Alisema kujengwa kwa viwanda ndani ya mji huo, kutasaidia kupunguza tatizo la upatikanaji wa ajira kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi na vitongoji vyake.

Shamba la mkonge la Kikwetu lililopo ndani ya Manispaa ya Lindi awali lilikuwa linamilikiwa na kampuni ya Amboni Estates Ltd halafu Tasco na baadaye Mohamed Enterprieses Tanzania Ltd ya jijini Dar es Salaam.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top