Featured

Loading...


Hatima ya Juma Duni Haji Kubaki CHADEMA Au Kurudi CUF kujulikana Januari


Mwanasiasa mkongwe nchini, Juma Duni Haji amesema hatima yake ya kubakia au kuondoka ndani ya Chadema itajulikana mwezi ujao.
Duni aliihama CUF na kujiunga Chadema ambayo ilimsimamisha kuwa mgombea mwenza wa urais wa Chadema iliyokuwa chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Vyama vingine vinavyounda Ukawa ni NLD na NCCR Mageuzi.
Tangu kuisha kwa Uchaguzi Mkuu na mgombea wa Chadema kushika nafasi ya pili,  Duni amekuwa kimya, lakini juzi alisema itakapofika Januari mwakani ataeleza mustakabali wake kisiasa.
“Kwa sasa sisemi jambo lolote, nitakuambia baadaye kidogo kama nitarudi CUF au nitabakia Chadema. Kuna mambo ninafanya kwanza, nisingependa kusema,” alisema Duni.
Pia, Duni alizungumzia hisia zake za kisiasa visiwani Zanzibar, akisema anashangazwa na kauli ya aliyekuwa Jaji Mkuu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Mark Bomani kumshawishi Maalim Seif Hamad akubali  uchaguzi urudiwe.
Siku chache zilizopita, Jaji Boman alinukuliwa na vyombo vya habari akimtaka Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar kukubali kurudia uchaguzi huo kama ilivyotangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salum Jecha kuwa utarudiwa ndani ya siku 90.
Jecha alifuta matokeo ya urais na uwakilishi wa Zanzibar, akisema kulikuwa na ukiukwaji wa sheria na kanuni na kwamba ndani ya tume yake wajumbe walitofautiana hadi kukunjana.
Jaji Bomani alisema kama Maalim Seif alishinda, atashinda uchaguzi ukirudiwa kwani wananchi watampigia kura.
Hata hivyo, Duni alisema: “Anajua kabisa nchi yoyote inaporudia uchaguzi mara nyingi amani huwa inapotea, kwa mfano Burundi leo hii bado wanauana na hakuna anayezungumza lolote kwa sababu ni chama tawala kimeshinda.
“CUF inasisitiza Katiba ya Zanzibar ilindwe au kwa sababu upande wa Bara wamepata Rais (John Magufuli), sasa hawajali usalama wa Wazanzibari?”
Duni alihamia Chadema chini ya mpango maalumu wa Ukawa wa kuwezesha vyama hivyo kuchukua urais Bara na Visiwani, mpango ambao haukuweza kuzaa matunda.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top