Featured

Loading...


Serikali Yafuta ‘Semina Elekezi’ Kwa Madiwani


Serikali imesema mafunzo kwa ajili ya madiwani wote hayatakuwepo na badala yake wenyeviti na makamu wa wenyeviti kote nchini ndio watapatiwa mafunzo ya namna ya kusimamia halmashauri zao.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) anayeshughulikia Utumishi na Utawala Bora, Selemani Jafo alisema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea Chuo cha Serikali za Mitaa cha Hombolo mjini Dodoma.

“Madiwani ni wengi wote kuwapatia mafunzo haiwezekani kila halmashauri itatoa mwenyekiti na makamu mwenyekiti, meya na naibu meya” alisema Jafo.
 Alisema mafunzo hayo yatahusisha wenyeviti wa halmashauri na makamu wao kutoka halmashauri 185 nchini na kuwaagiza wakurugenzi kuhakikisha viongozi hao wanafika Chuo cha Hombolo tayari kwa ajili kwa mafunzo hayo.

Alisema miaka ya nyuma kulikuwa na utaratibu wa kuwapatia mafunzo madiwani waliochaguliwa baada ya Uchaguzi Mkuu, lakini sasa ni wenyeviti na makamu wenyeviti wa halmashauri ndio watapatiwa mafunzo hayo.

Alisema halmashauri 185 zilizopo nchini zitapeleka watu wawili kila halmashauri na waliopata mafunzo hayo watakwenda kuwafundisha wengine.
 Naibu Waziri alisema kulikuwa na changamoto nyingi katika Uchaguzi Mkuu uliopita na madiwani walichaguliwa kutokana na sifa zao na wengine wananchi walifanya uchaguzi wa hasira, lakini mwisho wa siku kiongozi aliyetakiwa alipatikana.

Alisema madiwani wapya waliopatikana wapo wafanyabiashara, wanafunzi na watu wa kada mbalimbali ambao wote walitakiwa kufundishwa namna ya kutenda kazi zao.
 Hata hivyo, alisema mafunzo kwa ajili ya madiwani wote hayatawezekana, bali viongozi wa madiwani hao ndio watapatiwa mafunzo hayo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Serikali za Mitaa, Dk Emmanuel Gibai alisema maandalizi kwa ajili ya mafunzo hayo yamekamilika. 
Awali yalipangwa kutolewa kwa madiwani wote, lakini kutokana na maelekezo hayo wahusika watakaotakiwa kupatiwa mafunzo hayo watayapata.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top