Featured

Loading...


Taasisi 1,200 Duniani Zampa Tuzo ya Amani Edward Lowassa


Taasisi 1,200 duniani zitampa aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa Tuzo ya Amani kutokana na utulivu aliouonyesha kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu.
Akizungumza kutoka Bukavu, DR Congo, mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii, Mchungaji William Mwamalanga alisema Lowassa amechaguliwa jana mjini Bukavu na wajumbe 1,400 wa mkutano huo.
Mwamalanga alisema wajumbe wanaohudhuria kongamano la amani wanatoka mataifa ya Ulaya, Marekani, Asia na Afrika kwa kuwashindanisha wanasiasa 1,000 ili kumpata Kiongozi Bora wa Amani mwaka 2015, ambaye anajali na kuangalia maslahi ya jamii badala ya madaraka.
Hatua ya kumpatia tuzo Lowassa ni baada ya kuelezwa kuwa amedumisha amani hiyo hata baada ya kushindwa uchaguzi Mkuu wa Rais Oktoba 25.
Katika uchaguzi uliopita, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)ilimtangaza Dk John Magufuli kuwa mshindi kwa kupata kura 8,882,935 ikiwa ni asilimia 58.46 wakati Lowassa alipata kura 6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote.
Mchungaji Mwamalanga alisema katika kongamano hilo, wajumbe walijadili hali ya amani duniani na mchango wa wanasiasa katika kulinda amani hiyo.
Alisema kuwa wanasiasa barani Afrika wamekuwa vyanzo vya migogoro na mauaji ya raia wakati wa uchaguzi, kama ilivyo nchini Burundi. Hata hivyo, alisema kuwa wajumbe walipongeza ushindi wa Dk Magufuli, lakini wakasema umetiwa dosari na hali ya kisiasa Zanzibar baada ya matokeo kufutwa.
Alisema wajumbe wa kongamano hilo linaloshirikisha maaskofu, masheikh na vijana kutoka madhehebu mbalimbali ya dini barani Afrika, wamemuhimiza Rais Magufuli kumaliza utata wa uchaguzi wa Zanzibar.
Baada ya kupitishwa kugombea urais kwa tiketi ya Chadema, Lowassa alitangaza kuwa angefanya kampeni kistaarabu na kwa amani na baada ya matokeo aliwatuliza wafuasi wa chama hicho, akisema “hakuna anayeweza kuizuia bahati ya mtu” kwa hiyo kama amepangiwa kuwa rais, atakuwa.
Lowassa, ambaye ni Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne, aliongeza upinzani kwenye uchaguzi wa mwaka huu baada ya kuihama CCM na kujiunga na Chadema iliyoukuwa na nguvu ya vyama vingine vitatu vya NLD, CUF na NCCR-Mageuzi.
Kama alivyoahidi, Lowassa hakutumia mikutano yake ya kampeni kushambulia mambo binafsi ya wagombea wengine, bali muda mfupi kuomba kura.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top