Featured

Loading...


Mchina Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela Kwa Kuuza Bidhaa Bila Kutoa Risiti


Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemhukumu kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh4.5 milioni, mfanyabiashara Huifang Ma baada ya kupatikana na hatia ya kuuza bidhaa na kushindwa kutoa risiti kwa kutumia mashine ya kieletroniki. 
 
Ma ambaye ni raia wa China na mkazi wa Mtaa wa Narung’ombe eneo la Kariakoo, alihukumiwa kifungo hicho baada ya kukiri mashtaka mawili yaliyokuwa yakimkabili likiwamo la kushindwa kujisajili kulipa kodi ya ongezeko la thamani (Vat). 
 
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mwanadamizi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Said Mkasiwa alisema kwa kuwa mshtakiwa alikiri mashtaka yanayomkabili, anatakiwa kulipa faini au kwenda jela miaka mitatu. Hata hivyo, Ma alilipa faini na kuachiwa huru. 
 
Katika hati ya mashtaka, ilidaiwa kuwa Machi 23, mwaka huu eneo la Karikaoo, mshtakiwa alishindwa kutoa risiti za kieletroniki kwa mteja wake. 
 
Ilidaiwa kuwa siku hiyo mshtakiwa ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya HM Textile Co Ltd iliyopo Mtaa wa Agrey, Kariakoo, alishindwa kutumia mashine za EFDs kwa ajili ya kutoa risiti kwa wateja walionunua bidhaa dukani kwake.
 
Kosa la pili, mshtakiwa alishindwa kujisajili kama mlipa kodi wakati akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top