Featured

Loading...


Ofisa wa TRA na Mfanyakazi Mmoja wa Yono Auction Mart Wafikishwa Mahakamani Kwa Rushwa


Ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Amani Mkwizu na mfanyakazi wa kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Edward Magobela wamepandishwa kortini jana wakikabiliwa na mashtaka matatu ya rushwa. 
 
Washtakiwa hao walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakidaiwa kuomba rushwa ya Sh50 milioni na nyingine ya Sh5 milioni na kupokea Sh3 milioni kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Commercial Sales and  Services Tanzania Limited, Glenn Clarke. 
 
Akiwasomea mashtaka yao, Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Denis Lekayo alidai washtakiwa hao waliomba na kupokea kiasi hicho cha fedha ili kumwezesha mkurugenzi huyo kupunguziwa kodi aliyokuwa anadaiwa kutoka Sh375 milioni hadi Sh100 milion. 
 
Hata hivyo, washtakiwa hao walikana mashtaka na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika. 
 
Hakimu Huruma Shaidi anayesikiliza kesi hiyo, aliwaeleza washtakiwa hao kuwa dhamana yao iko wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili. Hata hivyo, walishindwa kutimiza masharti na kupelekwa mahabusu. 
 
Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 9 mwaka huu.
Awali, akiwasomea mashtaka, Wakili Lekayo alidai kuwa washtakiwa walitenda makosa hayo Aprili 19, mwaka huu, jijini Dar es Salaam kinyume cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Namba 7 ya mwaka 2011. 
Katika shtaka la kwanza, Wakili Lekayo alidai kuwa washtakiwa kwa pamoja na wengine ambao hawajakamatwa, waliomba rushwa Sh50 milioni kutoka kwa Clarke. 
 
Wakili Lekayo, alidai katika shtaka la pili washtakiwa hao kwa pamoja na wengine ambao hawajakamatwa bado, walijihusisha na vitendo vya kumuomba rushwa ya Sh5 milioni mkurugenzi huyo ili wampunguzie kodi kutoka Sh375 milioni mpaka Sh100 milioni. 
 
Katika Shtaka la tatu, Wakili Lekayo alidai washtakiwa kwa pamoja walijihusisha na vitendo vya rushwa kwa kupokea rushwa ya Sh3 milioni kutoka kwa Clarke ili wampunguzie kodi kutoka Sh375 milioni mpaka Sh100 milioni.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top