Featured

Loading...


MAGUFULI: Mafisadi Hawataki Niingie IKULU


MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli, amesema mafisadi hawawezi kumpigia kura katika Uchaguzi Mkuu ujao kwa kuwa wanamwogopa.
 
Dkt. Magufuli aliyasema hayo jana kwenye mkutano wa hadhara,uliofanyika katika Viwanja vya Mvumi Misheni, Jimbo la Mtera,mkoani Dodoma.
 
"Mafisadi hawawezi kunichagua kwa sababu wananiogopa ila wapo Watanzania wengi wanaonipenda na kunikubali wakiwemo maskini wenzangu, wanyonge ambao watanipa kura nyingi ili niweze kuwatumikia na kutetea masilahi yao," alisema.
 
Alimpongeza mwanasiasa mkongwe, Mzee John Malecela kwa ujasiri wake wa kuendelea kubaki CCM licha ya kushindwa katika mbio za kuwania nafasi ya urais miaka iliyopita.
 
"Mzee Malecela aliwahi kugombea uteuzi wa nafasi ya urais, lakini hakufanikiwa na hakufikiria wala kuthubutu kuhama chama hata siku moja, bado yupo na amekuwa msaada mkubwa," alisema.
 
Alisema mbali ya kuukosa urais, pia aliangushwa kwenye nafasi ya ubunge wa Jimbo la Mtera na Livingstone Lusinde lakini hakuhama chama. Alisema anawashangaa waliohama CCM baada ya kukosa nafasi.
 
Aliwaomba Watanzania wamchague aweze kubadilisha maisha yao na kukuza uchumi akiwataka wasikubali kudanganywa na wapinzani ambao hawana sera wala uzoefu wa kuongoza Serikali.
 
Akizungumzia sera ya elimu bure, alisema hakuna sababu ya kukosa madawati wakati nchi ina rasilimali kubwa ya miti; hivyo alitoa wito kwa Wakurugenzi kukaa mkao wa kufanya kazi.
 
Livingstone Lusinde
Naye Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM na mgombea ubunge Jimbo la Mtera, Lusinde alisema CHADEMA kimepoteza mwelekeo baada ya kuwapokea wanasiasa waliowatuhumu kwa kashfa mbalimbali ndani na nje ya Bunge.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top