Featured

Loading...


MBASHA ARUDISHWA KORTINI TENA

Brighton Masalu
SIKU chache baada ya kushinda kesi ya tuhuma za kubaka iliyokuwa ikimkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, mwimbaji wa muziki wa Injili, Emmanuel Mbasha anatarajiwa kupandishwa tena katika korti hiyohiyo kwa madai mengine, Risasi Mchanganyiko lina habari kamili.
Mwimbaji wa muziki wa Injili, Emmanuel Mbasha.
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni kwa sharti la kutotajwa jina, mmoja wa watu wa karibu na wanandoa hao, alisema Flora amefungua kesi ya madai ya talaka katika Mahakama ya Kisutu na kwamba muda si mrefu shauri hilo litaanza kusikilizwa.
“Flora ameenda mahakamani kudai talaka yake, kwa hiyo kesi inatarajiwa kuanza kusikilizwa muda wowote kuanzia sasa,” alisema mtoa habari huyo.Baada ya taarifa hizo, mwandishi wetu alimtafuta Mbasha kwa njia ya simu na kumuuliza juu ya madai hayo, ambapo alikiri na kudai anajiandaa kukabiliana na shitaka hilo.
“Yeah, ni kweli kaka, Flora ameamua kwenda mahakamani kudai talaka yake, sioni kama ni tatizo, kwa sasa siwezi kuzungumza lolote kwa sababu limeshafika katika mkondo wa sheria na tunapaswa kusubiri tuone kitakachotokea, lakini naamini kila kitu kitakwenda sawa,” alisema Mbasha.
Kwa upande wake, mke wa mwimbaji huyo, ambaye pia ni mkali wa nyimbo za gospo, Flora Mbasha alipotafutwa hakupokea simu yake ya mkononi, lakini alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms) alijibu kwa kifupi:
“Kaka, naendesha, kila kitu kiko mahakamani kwa hiyo sina la kuzungumza kwa sasa.”
Hali hiyo inatokea siku chache tu baada ya mahakama hiyo kumuachia huru mwimbaji huyo aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya ubakaji ambayo pia yalimleta mkewe huyo mahakamani akiwa shahidi wa upande wa mashtaka.
Kwa muda mrefu, waimbaji hao wamekuwa katika mgogoro wa kifamilia ambapo juhudi za watu mbalimbali zimefanyika kusuluhisha lakini hazikufanikiwa.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top