Featured

Loading...


Nape Azindua Kampeni ya NIMESHTUKA Ya Akina Ray Na Aunt Ezekiel Waliojitoa Chadema.....Akiri CCM Kuwa Na Mapungufu Kadhaa


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi CCM na mgombea ubunge Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amesema CCM haijakamilika kwa asilima 100 na kwamba kuna mambo machache ambayo hayako sawa lakini wanayafanyia kazi.

Nape amesema bianafsi anaupenda sana upinzani wa vyama vya siasa hapa nchini kwa kuwa wamekuwa wakiishtua Serikali ya CCM kwenye mambo machache ambayo yamekuwa yakilala ama kwenda kinyume na utaratibu.

Nape aliyasema hayo jana wakati akizindua Kampeni ya “Nimeshtuka” ambayo inawahusisha wasanii mbalimbali ambao awali walikuwa wanachama wa Chadema na kumuunga mkono mgombea urais wa Ukawa, Edward Lowasa ambapo kwa sasa wasanii hao wamehamia CCM.

Katika mkutano huo, Nape alibeza uamuzi wa Lowassa kuhamia Ukawa na kuongeza kuwa CCM imejipanga kushinda uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka huu.

Alienda mbali zaidi na kuwaomba wananchi kumuombea dua Lowassa aweze kuwa na afya njema ili Oktoba 25 aweze kushuhudia ushindi wanaoupata CCM.

Kwa upande wake kiongozi wa wasanii hao ambao wamejitoa Ukawa, Vincent Kigosi maarufu kwa jina la Ray alisema kuwa walipokwenda Ukawa walidhani wanakwenda kwenye safari ya matumaini hata hivyo baadaye waligundua safari hiyo haikuwa ya matumaini.

“Nimezunguka na Lowassa baadhi ya maeneo lakini sijaona sera za maana na zenye mashiko, nawaambia vijana wenzangu mimi nimeshtuka na nyie hebu shtukeni” amesema Kigosi.

Naye msanii wa filamu, Aunt Ezekiel aLIwataka vijana kujituma kwa kufanya kazi kwani hakuna mtu anayeweza kuwapa mabadiliko ya maendeleo isipokuwa ni vijana wenyewe.

ALIwashauri vijana kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kuichagua CCM badala ya kufuata mkumbo kwa kuamini ahadi zisizotekelezeka.

Wasanii wengine waliokuwemo kwenye Kampeni hiyo ni pamoja na Juma Nature, Inspekta Haroun ‘babu’, Kitale na wengine.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top