Featured

Loading...


Balozi Mwapachu arudisha Rasmi kadi ya CCM...... atangaza kujiunga UKAWA


Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kada wa CCM, Balozi Juma Mwapachu leo amerudisha kadi ya uanachama katika ofisi za CCM Kata ya Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Amesema anajiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) na kwamba baada ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 25 atatangaza chama anachojiunga miongoni mwa Chadema, NCCR-Mageuzi, CUF na NLD vinavyounda umoja huo.

Mwapachu amesema haoni sababu ya kutaja chama hicho sasa kwa vile lililo muhimu kwao hivi sasa ni umoja miongoni mwa wanamabadiliko na kujipambanua katika imani ya chama cha siasa hakuwezi kuwa na tija kwa umoja huo.

Amesema Lowassa anakwenda kuwa Rais wa Wanaukawa wote, hivyo watu wote wanaoamini katika mabadiliko ndani ya vyama hivyo wanapaswa kuwa wamoja kwa kuuwezesha umoja huo kuibuka na ushindi.

Akizungumza baada ya zoezi hilo, Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM mtaa wa Mikocheni A, Sudi Odemba amesema chama chake hakitapata madhara yoyote kutokana na hatua ya Balozi Mwapachu kijiengua na kutangaza kujiunga Ukawa.

Amesema Mwapachu hakuwa mwanachama aliyejitoa kukisaidia chama katika siku za karibuni na kwamba hajawahi kushiriki mikakati thabiti ya kukipatia CCM ushindi katika ngazi ya mtaa japo chama hicho kiliweza kuibuka na ushindi wa kishindo.

Jumanne wiki hii, Balozi Mwapachu alitangaza kujitoa CCM akikituhumu kukiuka misingi ya kidemokrasia wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais Julai mwaka huu ambapo Dk John Magufuli alichaguliwa huku mgombea anayeamini kuwa na maono ya kiuongozi kwa Tanzania ijayo, Edward Lowassa akikatwa.

TOA MAONI YAKO HPO CHN1 KUHUSU HABARI HII

KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU ...BASI BOFYA LIKE HPO CHINI KUUNGANA NASI KWENYE FACEBOOK

During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. During its two year run, the project will award approximately 100 major reporting grants and provide mentoring to support the best ideas for stories on development issues. Journalists who produce the best stories published or broadcasted in media that reach African audiences, will win a major international reporting trip. Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:.;

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright JICHO LETU
Back To Top